Friday, September 4, 2020

Salamu – Septemba, 2020

 Salamu – Septemba, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe. Ninakukaribisha tena katika eneo hili la salamu za mwezi. ili tupate kujifunza somo hili muhimu. Mungu ametupa mwezi huu wa tisa nani mwezi tunamshukuru sana.


Nimekuletea salamu za mwezi huu wa tisa. Kumbuka tunamfululizo wa salamu zenye kichwa.


MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)


JAMBO LA NANE JIFUNZE KUKIRI USHINDI KWA KINYWA CHAKO.


Mungu ili akuokoe katika majanga kama haya pia atataka kuangalia ukiri wako angalia mistari hii naamini utanielewa vizuri. “Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya. Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake naliona hasira, nikampiga; nalificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe. Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.” (Isaya 16-19)


Mungu anapokasirika na kuadhibu ili aponye fahamu ataangalia maneno yasemwayo na hao watu


Angalia vizuri hapo anasema atamponya huyo aliyempiga na kumletea amani kwa sababu Mungu anayaumba matunda ya midomo.


ILI UTOLEWE KWENYE MAUTI LAZIMA UJIFUNZE KUKIRI HUO WOKOVU


Angalia hii mistari uone: “Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” (Mithali 18:20-21)


Katika kipindi hiki unatakiwa ubadilike katika kusema kwako. *Anza kukiri huo wokovu usiseme  kwa kinywa chako kuwa utakufa.


Angalia mistari hii: “Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA.” (Zaburi 118:17)


Ukitaka upone majanga haya nakushauri jifunze kuukiri wokovu kutoka kwa Mungu. Angalia mistari hii “Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!” (Warumi 10:10-15)


Kile unacho kisema au kukikirifahamu ndicho kinaumbwa. katika ulimwengu wa roho fahamu wanafanyia kazi sana matamko yaliyosemwa na mtu au watu.


Iliuokoke leo na tauni au na jehanamu fahamu unatakiwa umuamini Bwana Yesu Kristo kuwa ndiye atakaye kuokoa. Sasa kwa mujibu wa hiyo mistari tunaona kuna mambo mawili hapo.


Jambo la kwanza ni kuamini moyoni,jambo la pili ni kusema au kukiri. Kwa nini unatakiwa ukiri? Kwa Mujibu wa hiyo Isaya na Mithali,unaona yakua wokovu umefungwa pia ndani ya kukiri kwa watu.


Jifunze kuisemesha nafsi yako katika kipindi kama hicho maneno kama haya. “Mkono wa kuume wa BWANA umetukuzwa; Mkono wa kuume wa BWANA hutenda makuu. Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA. BWANA ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.”(Zaburi 118:16-18).


Mwimba Zaburi hiyo aliyasema maneno hayo ya ya sintakufa bali ntaishi katika kipindi akitumikia adhabu iliyoletwa na Mungu


Kwanini alisema hivyo? Jibu ni rahisi tu, alitaka Mungu aumbe matunda ya kinywa chake ili apate wokovu asife katika adhabu hiyo.


Hata wewe ukikutana na kipindi kama hiki cha taifa au ulimwengu kuadhibiwa na Mungu, jifunze kusema maneno kama hayo mpendwa.


Usiseme tutakufa,au hatariiiii au mbona tunaishaa nk. Sema sitakufa bali ntaishi.


Naamini umenielewa mpendwa.


Mungu akubariki sana. Tuonane tena katika kona hii mwezi ujao.Naamini umenielewa sana.Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-


App yetu ya huduma yenye jina  “MWAKATWILA (HUSONEMU)” utaipata Play Store ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

YouTube – Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

Facebook ingia katika hiyo tovuti (website) yetu utaona alama ya Facebook (f) “like” na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”

DVDs au CDs

VITABU. Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-

Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.

Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.

Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-


+255 754 849 924 au +255 756 715 222


Wako


Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

Salamu – Agosti, 2020

 Salamu – Agosti, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Pole na hongera kwa kila jambo ulilokutana nalo mwezi uliopita. Tunamshukuru Mungu aliyetupatia nafasi hii ya kuuona mwezi huu mpya. Naamini katika mwezi huu kuna baraka ambazo Mungu ameziweka au kuzifunga ndani ya mwezi huu. Muombe Mungu akujarie kukutana nazo.


Nimekuletea salamu za mwezi. Naamini umekua ukibarikiwa na salamu za miezi iliyopita. Kumbuka tuna salamu zenye kichwa


MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)


JAMBO LA SABA JIFUNZE KUTOKUISHI KWA HOFU ISIYOFAA


Sikiliza ili leo hii upate kuokolewa na Mungu katika majanga ambayo chanzo chake ni tauni iliyoachiliwa na Mungu, ikiwa wewe ni kuhani na umewajibika kwa sehemu yako unatakiwa uhakikishe unaondoa hofu moyoni mwako ya kukutana na mauti hiyo iliyobebwa na tauni iliyoachiliwa na Mungu


KUNA HOFU AU WOGA WA AINA MBILI


Unaposoma maandiko matakatifu utaona ndani ya Biblia tunafundishwa kuwa kuna hofu za aina mbili;


HOFU INAYOTOKA KWA MUNGU


Angalia mistari hii: _“Basi tukiijua hofu ya Bwana, twawavuta wanadamu; lakini tumedhihirishwa mbele za Mungu. Nami natumaini ya kuwa tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia.” *(2 Wakorintho 5:11)


Angalia na mistari hii: “Tazama, nitatia roho ya hofu ndani yake, naye atasikia kivumi, na kuirudia nchi yake mwenyewe; nami nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.” *(2 Wafalme 19-7)


Hofu ni roho. Ukiipitia hiyo mistari hiyo utaona kuwa kuna hofu ya Bwana,ambayo hutoka kwa Mungu kabisa. Hofu hii Mungu huitumia kwa kazi nyingi tu.


Moja ya kazi ya hofu hii ni kuwafanya wanadamu wamwogope Mungu na kuacha matendo yao mabaya.


Angalia mfano huu angalia na mistari hii: “Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli. Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu. Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha. Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii. Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao (Zaburi 78:31-35)


Ukiipitia hiyo mistari utagundua kuwa Mungu anapoona wanadamu wamezidisha uovu juu ya nchi huchukua hatua ya kuwatiisha hao watu kwa jambo fulani ambalo ndani yake huibeba roho hiyo ya hofu na hofu hiyo maandiko husema huwashitua watu na watu hao ndipo huona umuhimu wa kumtafuta Mungu na kuacha njia zao mbaya.


TAUNI HUBEBA HOFU YA MUNGU NDANI YAKE


Mungu ana akili nyingi mnoo ya kutuvuta kwake ukiona majanga kama ya ya tauni fahamu ndani yake majanga haya hubeba hofu ya Mungu ndani yake.


Watu wanapokufa kwa tauni unajua ndipo wanadamu wengi huanza kumkumbuka Mungu na kumwogopa?


Wanadamu wengi huingia katika mashaka makubwa na mifadhaiko mingi mioyo yao hubeba huzuni n.k. Biblia inasema huzuni hubeba hofu na pia zipo huzuni za aina mbili pia


Angalia mistari hii: “Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu.Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.” (2 Wakorintho 2: 7-11)


Ukiipitia hiyo mistari utaona kuwa huzuni pia hubeba hofu. Hofu itokayo kwa Mungu huibeba  huzuni pia itokayo kwa Mungu. Mungu anapotuhuzunisha wanadamu kwa kutuletea hofu fahamu anachokitafuta ni kuona hao wanadamu wanatubia matendo yao.


Biblia inasema haya majanga yanapotokea huleta faida, angalia anasema “Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto;”


Mtu yeyote yule mwenye akili timamu hawezi kuendelea kufanya jambo ambalo anajua kabisa mwenzie kaadhibiwa tena kwa kuuawa. Mwenye akili ataliacha hilo jambo haraka sana. Na ataogopa kuendelea kulifanya.


Leo hii hofu hii ya Corona imewavuta watu wengi waanze kumkumbuka Muumba wao. Hata wale wanaomkumbuka wanajipanga vizuri kweli kweli. Ehehee!!


Ngoja nikukumbushe kitu. Kumbuka zamani ulipokuwa shule ya msingi siku ya mkaguo na iwe zamu ya yule mwalimu ambaye anafahamika kwa ukali mpaka shule ya tatu ambayo hajawahi hata kufundisha?


Wanafunzi woote siku hiyo huingiwa na hofu na kila mmoja utaona muda wa dakika chache tu alivyojifanyia usafi; iwe kwa mate, kwa kula kucha, kama nywele hakuchana na kichanio hakipo unajua hutafuta chelewa zinapangwa na kuwa kichanio siku hiyo mpaka nywele zionekane sawa.


Mungu anapowajilia wanadamu kwa mtindo huo wa kuwatia adhabu fahamu ndani yake hutaka kuona watu wakiwa na hofu ya kumwogopa.


Biblia inasema hivi: “Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.” (Zaburi 4:4)


Hii ni hofu ya Mungu inayotufanya sisi tusifanye dhambi. Ukimhofu Mungu au kumcha fahamu huwezi kutenda dhambi. Na hofu hii inaweza kubebwa na taarifa uliyoipata kuwa Mungu amewafanyia jambo fulani watu waliotenda dhambi, huwezi wewe ukatenda dhambi wakati wenzio wamepigwa.


Biblia inatufundisha kuwa tunatakiwa tuwakemee watu wadumuo kutenda dhambi mbele za watu ili watu wengine waogope. Angalia mistari hii: “Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.” *(1 Timotheo 5:20)


Kama Mungu anampa mwanadamu maarifa haya unafikiri yeye hawezi kuwaogopesha watu kwa kuyafanya mambo kama yayo hayo? Mungu huleta tauni ili tu kutujengea sisi wanadamu hofu ya kutokudumu katika kutenda maovu.


HOFU ILETAYO MAUTI AU MABAYA


Pia Biblia inatufundisha kuwa kuna hofu ambayo chanzo chake si Mungu. Na hofu hiyo inaweza kumsababishia huyo mwenye hofu kukipata kitu hicho kibaya anachokiogopa.


Angalia mistari hii: “Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.” (Mithali 10:24)


Ukiipitia hiyo mistari utagundua kuwa. Haikupasi ndugu kuwa na hofu ya kupatwa na tauni. Kwa mujibu wa mistari hiyo tunafundishwa kuwa ili tusipatwe na tauni au jambo baya tunatakiwa tuhakikishe hatukiogopi hicho kitu.


Sikiliza mwogope Mungu, usiogope kitu kingine. Angalia hii mifano: “Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu. Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.” (Mithali 3:24-25)


Unapoona kuna mambo kama hayo wewe mpendwa unatakiwa usiingize hofu yoyote.


JENGA IMANI YA KUOKOLEWA KATIKA JANGA HILI


Kumbuka unapopata hofu ni rahisi kujikuta unakutana na hicho, unachokiogopa.


Mfano, angalia umesikia habari za tauni yoyote au nzige au vita yaani upanga moyoni mwako unalitazamaje hili jambo?


Wewe ni kuhani, mwombezi unatakiwa uhakikishe unajenga imani moyoni mwako ya kuokolewa na Mungu katika janga hili.


Usiogope na kujaa mashaka na kukosa amani kisa eti umesikia tauni ya aina yoyote ile inaua wazee, vijana, nk.


Ili uokolewe unatakiwa ujifunze kutokuwa na mashaka. (SINA MAANA USICHUKUE HATUA YOYOTE UTAKAYO AMBIWA NA SAREKALI) Ninachotaka kukujengea ni hiki usiogope amini kuokolewa hata kama ukikutana nao.


Kwa nini uwaze kufa wakati kuna watu wameugua tauni hiyo na umewaona wamepona? Kwa nini ufikiri utaambukizwa wakati kuna watu wengi tu wapo katika nchi iliyojaa tauni hiyo na hawajaambukizwa?


KAA MBALI NA MTU AKULETEAYE MANENO YA HOFU


Biblia inasema hivi: “Tena maakida na waseme zaidi na watu, wawaambie, Ni mtu gani aliye hapa tena mwenye hofu na moyo mnyonge? Aende akarudi nyumbani kwake, isije mioyo ya nduguze ikayeyuka mfano wa moyo wake.” (Kumbukumbu la Torati 20:8)


Ukiipitia hiyo mistari utaona hiki ninachokuambia. Mtu ambaye ana moyo wa hofu haifai kukaa naye karibu. Atakuambukiza hiyo roho ya kuogopa.


HOFU AU MASHAKA NI SUMU YA IMANI


Unapomwomba Mungu akuokoe na tauni unatakiwa ujenge imani ya kuokolewa wewe na nyumba yako na taifa lako. Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo.


Jenga uhakika moyoni mwako ya kuwa Mungu ameokoa. SIYO ATAKUOKOA NASEMA AMEKUOKOA.


Ukijenga imani hiyo fahamu hautazama ndani ya tauni. Angalia mifano hii: _“Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.  Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?” (Mathayo 14:22-31)


Ukiipitia hiyo mistari utakigundua hiki ninachokuambia. Kilichomfanya Petro azame ni hofu ya maji. Fikiria alianza kutembea juu ya maji. Fikiria mwokozi yupo na ndiye amemwambia njoo yeye aliona shaka!!


Shaka ndiyo sumu ya imani. Na sisi tunaokokewa kwa imani. Hata hili janga tunaokolewa kwa imani.


Ondoa woga amini umeokolewa mpendwa!!! Usiangalie unasikia nini wangapi wamekufa wangapi wameambukizwa n.k.


Katika kipindi watoto wa Mungu wengi hujikuta wakiacha hata kufanya kazi ya kuwaingizia kipato kisa eti hofu ya tauni.. Usihofu ondoa masikio yako kusikia habari za kukutisha tamaa.


Fanya kazi zako kama kawaida, panga mipango yako kama kawaida. Mwenye kwenda shamba nenda shamba. Ngoja nikuchekeshe, katika kipindi cha corona 19, tauni hiyo ilikua ikileta mafua yaani tatizo la upuaji.


Fikiria mtu anahofu, na akapita kwenye vumbi hivi au akapita kwenye eneo la watu wanaopaka ukuta rangi, ni rahisi kujikuta ana mafua, sasa hapooo!!


Nirahi mpendwa kuanza kuwasumbua watu tu na wauguzi. Kisa hofu ya tauni hiyo.


“Nirahisi kila waki kusema hivi Ohoooo! Nahisi ninao!!!” Sikiliza ukikutana na hali hiyo ondoa hofu mpendwa, yamkini ni mafua ya kawaida tu. Fikiria ndiyo umekutana na mtu ana mafua tu. Hapo sasa? Niliwaona watu wengi wakiwaogopa watu sana.


Usishangae kwa ajili ya hofu watu wengi walishuka kwenye magari au bajaji, kisa waliogopa tauni ya Corona, ukifikia hali hiyo mpendwa wewe sasa ni mtumwa na ni mtu asiye na imani kwa Mungu wake.


Hebu angalia ahadi ya Mungu katika maneno haya. “Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita. Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi. Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;  Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?” (Zaburi 56:1-4)


Angalia na mistari  hii mingine.“Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini. Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo. Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao. Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana, Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri, Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe. Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki. Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.” (Zaburi 91:1-11)


Sikiliza keti na Mungu kaa chini ya uvuli wake yaani jiachie kwake utaokolewa na tauni mpendwa. Usihofu sasa. Fanya unayoweza kufanya lakini jenga matumaini yako kwake. Matumai ya kuwa Bwana Yesu Kristo kukuokoa.


Mungu akubariki sana. Tuonane tena katika kona hii mwezi ujao.Naamini umenielewa sana.Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-


App yetu ya huduma yenye jina  “MWAKATWILA (HUSONEMU)” utaipata Play Store ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

YouTube – Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

Facebook ingia katika hiyo tovuti (website) yetu utaona alama ya Facebook (f) “like” na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”

DVDs au CDs

VITABU. Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-

Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.

Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.

Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-


+255 754 849 924 au +255 756 715 222


Wako


Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

Salamu – Julai, 2020

 Salamu – Julai, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana, Mimi na familia yangu ni wazima. Tunamshukuru Mungu. Nimekuletea mfululizo wa salamu za mwezi.


Tuna salamu zenye kichwa


MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)


Katika salamu za mwezi uliopita tuliangalia jambo, la sita nalo lilikua JAMBO LA SITA ACHA KUFANYA MAOVU ILI MUNGU ASIKUPIGE NA TAUNI.


Hebu tuendelee mbele kidogo. Mara nyingi tauni inapotokea wanadamu wanaingia hofu sana. Na hofu kuu ipo kwenye kufa. Wengi huingia kutubu.


Sikia toba lazima iende na geuko. Kama hakuna geuko au watu hawajabadili tabia fahamu ni ngumu Mungu kuponya au kuiondoa hiyo tauni.


MFANO TUNAOMBA TOBA NA NI TOBA YA MUNGU KUTUSAMEHE DHAMBI . NIKUULIZE SWALI , JE! AKITUSAMEHE DHAMBI HARAFU? Utasema aondoe ugonjwa, akiondoa harafu?


Lazima tumhakikishie tuna acha dhambi. Na tumhakikishiye kuwa tunaacha dhambi kiukweli, Mfano wa kumdanganya.


Angalia mfano huu wa hawa ndugu walitubu lakini hawakua wakweli. “Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli. Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu. Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha. Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii. Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao. Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao. Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake. Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote. Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.”(Zaburi 78:31-39).


Ukiipitia hiyo mistari utagundua kuwa hao ndugu walitubu ili Mungu asiwaue, lakini hawakutaka kubadilika tabia, hata waliposema wanatubu walikua waongo. Kilichowasaidia ni ile rehema ya Mungu tu.


Mungu anapoleta tauni na hiyo tauni ikaanza kuua watu fahamu ndani yake anataka kuona watu wakilijua kosa lao na waliungame na wageuke kwa kuacha dhambi ambazo ndiyo chanzo cha tauni au nzige hao.


Sikiliza Mungu anapokasirikia wenye dhambi na hao wenye dhambi wakijua kosa lao na kugeuka na kuziacha njia zao mbaya Mungu huwaokoa hao watu na tauni.


Hebu ona mfano huu wa nini ufanye ikitokea tauni, Mungu anasema tutubu na tumludie kwa mioyo yetu yoote.


“Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; Wenyeji wote wa nchi na watetemeke; Kwa maana siku ya BWANA inakuja. Kwa sababu inakaribia; siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza kuu. Kama mapambazuko yakitandazwa juu ya milima, hao ni wakuu, tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi. Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na bustani ya Adeni mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao. Kuonekana kwao ni kama kuonekana kwa farasi; na kama wapanda farasi ndivyo wanavyopiga mbio. Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita. Mbele yao watu wanahangaika; nyuso zote zimegeuka kuwa nyeupe kwa hofu. Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita; nao huendelea mbele kila mmoja katika njia zake, wala hawapotoshi safu zao.Wala hapana mmoja amsukumaye mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake; hujifanyizia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata njia yao. Huurukia mji; hupiga mbio juu ya ukuta; hupanda na kuingia ndani ya nyumba; huingia madirishani kama aingiavyo mwivi. Nchi inatetemeka mbele yao; mbingu zinatetemeka; jua na mwezi hutiwa giza, na nyota huacha kuangaza;naye BWANA anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya BWANA ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili? Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa BWANA, Mungu wenu? Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake. Hao makuhani, wahudumu wa BWANA, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee BWANA, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao? Hapo ndipo BWANA alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake.”(Yoeli 2: 1-18).


Ukiipitia hiyo mistari kumi na nane utaona wazi kuwa Mungu akikasirika anawatuma hao amewaita jeshi lake ili wawaue wanadamu. Hiyo ni tauni na nzige.


Inapokuja hakuna anayeweza kuizuia. Ili izuiliwe mwenye uwezo huo ni Mungu tu, na ameweka utaratibu wawanadamu wafanye nini ili Mungu aizuie hiyo tauni.


Amesema wamludie, tena WAMLUDIE KWA MIOYO YAO YOOTE. Kwa maana nzuri waache dhambi,watubu na walie mbele zake. Ndipo huliondoa hilo jeshi lake lake la ajabu.


Naamini umenielewa sana.Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-


App yetu ya huduma yenye jina  “MWAKATWILA (HUSONEMU)” utaipata Play Store ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

YouTube – Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

Facebook ingia katika hiyo tovuti (website) yetu utaona alama ya Facebook (f) “like” na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”

DVDs au CDs

VITABU. Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-

Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.

Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.

Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-


+255 754 849 924 au +255 756 715 222


Wako


Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

Salamu – Juni, 2020

 Salamu – Juni, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Ni imani yangu kuwa Mungu amekupa uzima. Mi mi na familia yangu ni wazima tunamshukuru Mungu.


Nimekuletea salama za mwezi wa sita. Naomba zipokeee. Kumbuka tunasomo lenye kichwa


MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)


JAMBO LA SITA ACHA KUFANYA MAOVU ILI MUNGU ASIKUPIGE NA TAUNI


Sikiliza maneno haya: “BWANA akamtokea Sulemani usiku, akamwambia, Nimesikia uliyoyaomba, na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu. Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.” (2 Mambo ya Nyakati 7: 12-15)


Unapoisoma hiyo mistari utaliona hili jambo ninalokuambia, Maandiko yanasema: “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.”


Moja ya jambo ambalo Mungu ataliangalia ili aondoe tauni au nzige nk ni hili la hao waliomwudhi mpaka akaamua kuwaua kwa tauni wameamua kuacha matendo yao mabaya  ambayo kwa kweli yalikuwa yanamwudhi Mungu.?


Angalia mwenyewe hapo anasema wakiaziacha njia zao mbaya. Kwa mujibu wa hiyo mistari, hebu mwulize swali ikiwa hatutaziacha njia mbaya itakuwaje?


Jibu ni rahisi tu haondoi tauni au haponyi nchi.


Ili Mungu ainusuru nchi na janga hili kila mwenye mamlaka yoyote iwe kisiasa au kidini lazima awaambie watu wa nchi yake ukweli KUWA KILA MTU AACHE DHAMBI. NAWAAMBIA UKWELI HILI NDILO LITASAIDIA MNOO KULIKO JAMBO LOLOTE


UKITAKA MUNGU AKUOKOE KATIKA KIPINDI KAMA HIKI NI LAZIMA WEWE MWENYEWE UMHAKIKISHIE KUWA UTABADILIKA KATIKA MWENENDO WAKO.


Sikiliza ukitaka Mungu akuokoe wewe au watu wako, ni lazima pia uhakikishe kuwa unamhakikishia kuwa utabadilika kwa kuyaacha mambo yako yaliyo maovu au umhakikishie kuwa utafanya jitihada kubwa ya kuwashawishi hao unaowaombea waache tabia zao mbaya.


Ngoja nikupe mifano hii mizuri angalia mistari hii“Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao. Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo. Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo. Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate. Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu? Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate” (Luka 13:1-9)


Ukiisoma hii mistari utanielewa haraka mno nakufundisha nini. Hao ndugu walisikia namna watu hao walivyokutwa na magumu yaliyobebwa na mauti.


Na unapoisoma hiyo mistari utagundua hao watu walikufa kwa sababu ya matendo yao maovu. Bwana Yesu Kristo aliwaonya hao ndugu waliokuwa wamesikia kilichowapata wenzao kuwa hata wao wako kwenye hatari kama hiyo hiyo.


Ili hatari hiyo isiwapate aliwafundisha neno hili watubu.


TOBA ISIYO NA GEUKO HIYO SIYO TOBA


Fahamu ndani ya neno toba kuna kugeuka au kuacha kuyafanya yale maovu ya zamani. Kwa maana nzuri ni hii ili Mungu amwokoe mtu na tauni au gumu lolote linalotokana na hasira yake ni lazima huyo mtu au hao watu watubu au waache njia zao mbaya. Toba isiyo na geuko hiyo siyo toba.


Unapoisoma hiyo mistari utaona huyo mtu ambaye alisimama ili kuunusuru huo mti usikatwe alimshawishi huyo mwenye mti asiukate kwa sababu moja tu kubwa, kuwa mti huo kuanzia sasa utaanza kuzaa matunda.Kwalugha huo mti unaachana na tabia yake ya kwanza ya kutokuzaa matunda


Kwa maana nzuri zaidi mti huo utaacha mwenendo mbaya wa zamani na kuanza mwenendo mpya wa kuzaa matunda, fahamu mti huo ulipewa mwaka mmoja, mti huo ulitakiwa ndani ya mwaka huo mmoja ubadilike, usipobadilika katika kipindi hicho unakatwa.


Sikiliza katika kipindi kama hicho itategemea kasi ya tauni hiyo au nzige iliyopelekwa ulimwenguni ina kasi kwa kiwango gani. Kama kasi ni kubwa usifikiri hapo umepewa mwaka wa kubadilisha mfumo mzima wa maisha yako mpendwa.


Fikiria kidogo kipindi hicho mfano una mwomba Mungu usiugue ugonjwa huu, na inawezekana kabisa umekutana na hiyo tauni fahamu hapo kuna mambo mawili pia kuna kufa au kupona, swali langu unafikiri unatakiwa ufanye nini ili umshawishi


Mungu ili akuponye? KUMBUKA MPENDWA TAUNI IKILETWA KUNA KUWA HAKUNA DAWA.


Kama hakuna kinga na hakuna dawa maana yake TUNAMHITAJI MUNGU KWA UHITAJI MKUBWA.


Unafikiri ili kumwomba akupe siku nyingine yaani akukinge usipate, au akuponye unatakiwa umwambie neno gani zito hapo?


Rudi kwenye maneno yake aliyosema, anasema wakiziacha njia zao mbaya nitawaponya. Kwa hiyo kumbe tauni inapoletwa na Mungu, ina tabia ya kuwakwepa watu ambao wamefanya maamuzi thabiti moyoni ya kubadilika.


Na mtetezi wao ni mmoja tu ni Bwana Yesu Kristo ambaye atarudi kwa Mungu na kumwambia Baba huyu ndugu hebu tumwache tumpe siku kadhaa ameahidi kubadilika yaani kuzaa matunda.


Natamani unielewe mpendwa shoka limewekwa mtini, wewe ndiyo mti, ili usikatwe angalia hoja yako kwa mkataji unamwambia nini? Mwambie niache usinikate na ahidi nitakuzalia matunda yaani NABADILIKA KUANZI DAKIKA HII.


Angalia mfano huu uone ambao Yohana mbatizaji aliusema kwa watu ambao walikuwa wanajaribu kuikimbia adhabu ya Mungu, aliwaambia hivi: “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba; wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.” (Mathayo 3:7-10)


Maandiko yanatupa akili hapo kuwa kipindi kama hicho kikimkuta mwanadamu anatakiwa ahakikishe anaikwepa hasira ya Mungu kwa kukimbilia kubadilika tabia yaani aache mwenendo wake mbaya.


Angalia mfano huu uone alichowaeleza Yohana hao watu wakifanye: “Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi? Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo. Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi? Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa. Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.” (Luka 3:9-14)


Yohana aliwajibu hao watu kwa kuwafundisha ni nini wanatakiwa wakifanye katika kipindi cha kukabiliana na hasira ya Mungu.


Aliwaambia waache uovu. Waache tabia zao mbaya. Sikiliza mpendwa unapokutana na janga la tauni ulimwenguni unatakiwa ufanye nini? Umemsikia Mungu hapo akupavyo akili ili akuponye na kukuokoa na tauni anataka uache huo uovu wako?


Basi mnyenyekee. Mwambie kwa kimywa kuwa umemkosea sana. Lia mbele zake. Mwambie kuwa UNAACHA MWENENDO MBAYA.


Anza sasa hivi kuuacha huo mwenendo. Mfano leo hii acha uzinzi, acha ulevi, acha sigara, sikia nikuambie Virusi vya tauni kama corona inawaua mno watu wenye tabia hizi. Mimi najua ninachokuambia. Mzinzi, mlevi, mtu wa sigara, madawa ya kulevya, n.k. ni ngumu kupona ukipata.


Unajua kwa nini? Yaani vitu hivyo vinaondoa mnoo nguvu ya kinga za mwili. Acha tabia ya uongo, acha kubambikizia watu kesi, umemsikia Yohana akiwaambia askari? Hiyo ni tabia ya dhambi mpendwa


Acha kuabudu miungu, leo hii ondoa hirizi, n.k. havitakulinda nakuambia.


Acha kuiba, acha kuiibia pia serikali kwa kulipa kodi au ushuru kuanzia sasa


Mwambie Mungu nitatosheka na mshahara wangu, acha kuiba mpendwa. Kumbuka sana hili badilisha mfumo wa tabia yako hili litakusaidia mnoo katika kuokolewa na shoka lililowekwa tayari ili kuukata mti yaani wewe.


Mungu akuwezeshe kunielewa na kuchukua hatua.


Tuonane katika katika salamu za mwezi ujao.


Ubarikiwe sana pia ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-


Website yetu ya www.makatwila.org

Youtube- Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU

Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga

Dvds au Cd

Vitabu

Kwa njia ya Redio mbalimbali Rungwe fm102.5 Kila siku Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku

na Baraka Fm107.5 kila siku ya jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku na Bomba fm 104.1 kila siku ya ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku 7: Unaweza kutupata kwenye redio yetu online ya. radio.mwakatwila.org

Kwa mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi. 0754849924, 0756715222


Wako Mr &Mrs Steven Mwakatwila

Salamu – Mei, 2020

 Salamu – Mei, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Ndugu zangu niwape pole kwa na,na taifa na ulimwengu tunavyopitia kutokana na janga la corona.


Niwape pole wote mliougua,au kufiwa na ndugu na jamaa kwa ajili ya jambo hili. Tuendelee kumsihi Mungu sana ili atuvushe salama katika janga hili.


Kwa kuwa mwezi wa nne serekali ilikataza makusanyiko hata sisi tumesimamisha ratiba yetu yoote ya semina mbalimbali ambazo ilikua tuzifanye. Nikuletea salamu za mwezi wa tano.


Tunasalamu zenye kichwa hiki


MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)


Mwezi huu nataka tuendelee mbele kidogo. Tuangalie jambo la tano muhimu.


JAMBO LA TANO: JIFUNZE KUOMBA MUNGU AONDOE ADHABU


Angalia mistari hii: “BWANA akamtokea Sulemani usiku, akamwambia, Nimesikia uliyoyaomba, na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu. Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.” ( Mambo ya Nyakati 7: 12-15)


Ukiipitia hiyo mistari utaona Mungu anaahidi hapo kuwa, watu wake walioitwa kwa jina lake wakijinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wake na kuziacha njia zao mbaya anasema atasikia, na kusamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao.


Anaposema kuiponya nchi yao maana yake ni kuwa ataondoa tauni au nzige na kuwarudishia hao watu afya na kuwapa chakula tena.


Sasa sikia, unapomwendea Mungu kama kuhani katika eneo la kuomba toba, lazima tujifunze pia kumwomba na kumbembeleza kwa kilio ili aondoe adhabu aliyoipeleka.


UTOFAUTI WA TOBA YA UPATANISHO NA TOBA YA KUONDOA ADHABU


Kuna utofauti sana tu wa toba ambayo ndani yake imelenga kumwomba Mungu aondoe adhabu na toba ambayo ndani yake imelenga kufanya upatanisho kati ya Mungu na wanadamu.


Angalia mistari hii naona utanielewa nasema nini: “Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu. Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu? Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako. Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele. Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.” (Kutoka 32:9-14)


Ukiipitia hiyo mistari utaona alichokuwa anakishughulikia Musa ni toba iliyolenga kuondoa adhabu.


Musa alijua kuwa Mungu kakasirika na kaamua kuwaua hao watu. Mungu alimwambia kabisa Musa kuwa na waua wote nakubakiza wewe tu. Musa akaamua kufanya toba maalumu akimsihi Mungu aondoe adhabu hiyo aliyoiweka dhidi ya wana wa Israeli.


Fikiria Musa aliutafuta uso wa Mungu katika toba ya namna hiyo kwa muda wa siku arobaini. Mungu alikubali kuondoa adhabu. Lakini hakuwa tena patano au ushirika na wana wa Israeli.


Unaweza kujiuliza ulijuaje kuwa hakuwa na ushirika au patano nao?


Angalia katika kitabu hicho hicho hapo chini kidogo maandiko yanasema hivi: “Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, Mmetenda dhambi kuu; na sasa nitakwenda juu kwa BWANA, labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu. Musa akarejea kwa BWANA akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu. Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika. BWANA akamwambia Musa, Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu. Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake; tazama, malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.  BWANA akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Haruni aliifanya.” (Kutoka 32:30-35)


Hebu itazame kwa makini mistari hiyo. Utagundua kuwa Musa alirudi tena kwa Mungu kwa kazi maalumu ya kuwapatanisha au kuurejeza ushirika uliopotea kati ya Mungu na hao wana wa Israeli.


Sikiliza toba ile ya kwanza na hii ya pili hazifanani kabisaa. Toba ya kwanza Musa alishughulikia adhabu iondolewe. Toba ya pili alishughulikia upatanisho kati ya Mungu na wana wa Israeli.


Mfano Angalia Tena mistari hiyo shuka chini kidogo utaona Mungu anasema hivi:


“BWANA akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii; nami nitamtuma malaika aende mbele yako; nami nitawafukuza Mkanaani, na Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi; waifikilie nchi imiminikayo maziwa na asali; kwa maana mimi sitakwenda kati yenu; kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu; nisiwaangamize ninyi katika njia. Watu waliposikia habari hizo mbaya wakaomboleza wala hapana mtu aliyevaa vyombo vyake vya uzuri.” (Kutoka 33:1-4)


Mungu aliwasamehe hao watu kwa kuwaondolea adhabu. Lakini alikataa kwenda nao au aliondoa ushirika kati yake na hao wana wa Israeli. Wana wa Israeli walijua kabisaa kuwa wamesamehewa adhabu ya kifo hawatakufa lakini Mungu hatakuwa nao tena katikati yao.


Wakalia na kuomboleza sana, walijua kitendo cha kuto kuongozana na Mungu ni janga kubwa mno.


Musa ikabidi aingie tena kwenye maombi mazito ya toba na kumwomba Mungu aende nao au awe katikati yao. Mungu alikubali.


Hata leo tunapoomba toba kwa ajili ya Corona au nzinge au tauni ya aina yoyote ile ulimwenguni, makuhani wa Bwana lazima pia tumsihi aondoe adhabu. Tunaweza kuomba msamaha, akatusamehe kabisaa lakini adhabu ikabaki pale pale, mpaka tutakapoanza kumlilia kuwa ondoa adhabu


Angalia mfano huu uone: “Basi Nathani akamwambia Daudi, Wewe ndiwe mtu huyo. BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nalikutia mafuta, uwe mfalme juu ya Israeli, nikakuokoa na mkono wa Sauli; nami nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake za bwana wako kifuani mwako; nikakupa nyumba ya Israeli na ya Yuda; na kama hayo yangalikuwa machache, ningalikuongezea mambo kadha wa kadha. Kwa nini umelidharau neno la BWANA, na kufanya yaliyo mabaya machoni pake? Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, nawe umemtwaa mkewe awe mke wako, nawe umemwua huyo kwa upanga wa wana wa Amoni. Basi, sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, kuwa mke wako. BWANA asema hivi, Angalia, nitakuondokeshea uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako mbele ya jua hili. Maana wewe ulifanya jambo lile kwa siri; bali mimi nitalifanya jambo hili mbele ya Israeli wote na mbele ya jua. Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa. Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umewapa adui za BWANA nafasi kubwa ya kukufuru, mtoto atakayezaliwa kwako hakika yake atakufa. Naye Nathani akaondoka kwenda nyumbani kwake. Basi BWANA akampiga yule mtoto ambaye mkewe Uria alimzalia Daudi naye akawa hawezi sana. Basi Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya mtoto; Daudi akafunga, akaingia, akalala usiku kucha chini. Nao wazee wa nyumba yake wakaondoka, wakasimama karibu naye, ili wamwinue katika nchi; lakini hakukubali, wala hakula chakula pamoja nao. Ikawa siku ya saba, yule mtoto akafa. Nao watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia ya kuwa mtoto amekufa, maana, walisema, Angalieni, yule mtoto alipokuwa angali hai, tulisema naye, asitusikilize sauti zetu; basi hatazidi kujisumbua, tukimwambia ya kuwa mtoto amekufa?” (2 Samweli 12:7-18)


Unapoisoma hiyo mistari utajifunza kwa upana kidogo hiki ninachokufundisha.


Mfalme Daudi alifanya dhambi, dhambi hiyo ilipofanywa Mungu aliamua kumwadhibu.


Adhabu haikuwa moja, ilikuwa nyingi sana, mojawapo ni ya yeye kufa. Mfalme Daudi alipotubu dhambi yake hiyo unaona Mungu alimwambia hivi: “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.”


Najifunza kitu hapo, mfalme Daudi alishughulikia dhambi na pia alishughulikia adhabu yake ya kifo. Mungu alimsamehe akaondoa dhambi akamwondolea na adhabu ya kifo.


Kuna kitu kingine cha kujifunza hapo, Daudi hakufanya toba ya kuondoa adhabu ya upanga na tendo la wakeze kulala na mtu mwingine. Hakufanya hivyo.


Cha ajabu mfalme Daudi alishughulikia adhabu ya kifo cha mtoto wake mtarajiwa ambaye alimpata ki-uzinzi na kuua watu. Mungu hakumsikiliza kabisa adhabu ilibaki palepale. Mtoto alikufa.


Ninachotaka nikutazamishe ni hiki. Fikiria kidogo kama Daudi angefunga na kumlilia Mungu ili aondoe adhabu ya upanga na wakeze kulala na mwanaume mwingine unafikiri Mungu angefanyaje? Mimi naamini angesikia.


Mfalme Daudi hakuwa na mzingo wa watoto wake wengine kukumbana na kifo cha upanga na wakeze kubakwa, akawa na mzingo wa mtoto wake mmoja tu tena aliyesababisha magumu hayo yoote.


Mungu hakumsikia, Daudi aliwabagua hao wengine hakuona umuhimu wa kuwalilia, Mungu na yeye akamnyamazia.


Nataka utanue wigo wa fikra zako, kuhani wewe usiwe mbaguzi unapoombea maombi ya Mungu kuondoa adhabu.


Walilie watu woote ili Mungu awaondolee adhabu. Usifikiri Mungu anataka watu fulani wafe. Mungu hapendi mtu yeyote apotee bali kila mtu afikilie toba.


Angalia tauni inavyoua watu. Wengi wanaokufa hawamjui Bwana Yesu Kristo. Kuhani mwenye akili hawezi kuwabagua hao.


Anza leo kushughulikia pia maombi maalumu Mungu aondoe adhabu.


Naamini umenielewa.


Ubarikiwe sana na ufanyie kazi somo hili


Tuonane katika katika salamu za mwezi ujao.


Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-


App yetu ya huduma yenye jina  “MWAKATWILA (HUSONEMU)” utaipata Play Store ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

YouTube – Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

Facebook ingia katika hiyo tovuti (website) yetu utaona alama ya Facebook (f) “like” na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”

DVDs au CDs

VITABU. Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-

Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.

Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.

Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-

+255 754 849 924 au +255 756 715 222

Wako

Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

Wednesday, May 13, 2020

Salamu – Aprili, 2020

Salamu – Aprili, 2020

Ninawasalimu wapendwa woote katika jina la Bwana Yesu Kristo. Tunamshukuru sana Mungu ambaye ametupa mwezi huu wa nne. Naamini unajua kabisa kuwa kupewa mwezi mwingine ni neema kubwa mno.

Hasa katika kipindi hiki ambacho dunia inapitia janga kubwa la tauni ya Corona. Na hapa nchini imefika na tayari watu wengi wameambukizwa na wengine wamefariki na serikali imetoa utaratibu wa nini kila mtu afanye ikiwemo kunawa, kutokukaa kwenye mikusanyiko na hata vyuo na shule zote kufungwa.

Ni kipindi kigumu mnoo, nchi zingine wamefungiwa watu ndani kwa kupewa amri ya kutokutoka nje. Tunashukuru serikali yetu imeweka utaratibu wa kila mtu afanye kazi na pia imeruhusu ibada. Hili ni jambo la kumshukuru Mungu sana.

Somo hili ambalo tunalipata hapa linaweza kukusaidia sana katika kipindi hiki. Ngoja nikupe taarifa fupi ya mwezi uliopita. Mwezi uliopita tulikuwa na semina Bethlehemu na Mbalizi Bethani KKKT. Semina hii tulianza nayo mwishoni mwa mwezi wa pili na tukaendelea nayo mpaka tarehe tano mwezi wa nne.

Ninapokuletea salamu hizi nipo jijini Mbeya kwa sababu ratiba yetu ya mwezi huu ilikuwa tuwe Dodoma na Manyoni. Kutokana na mambo yaliyo nje ya uwezo wetu semina hizi tumeziahirisha.

Hiyo ndiyo taarifa fupi ya huduma mwezi uliopita. Hebu tusogee mbele kidogo katika salamu za mwezi huu. Kumbuka tuna salamu zenye kichwa.

MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)

Tuangalie jambo la tano

JAMBO LA TANO: JIFUNZE KUFANYA TOBA BILA KUANGALIA UKAMILIFU WOWOTE

Sikiliza, Unapomwendea Mungu katika kipindi hiki cha kumwomba kwa ajili ya wokovu wa tauni au nzige, n.k. iliyopelekwa na Mungu, unatakiwa wewe kama kuhani uhakikishe moyoni mwako unaondoa ile hali ya kujiona uko msafi.

Angalia mistari hii uone: “Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi.Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki. Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;” (Waebrania 5:1-7)

Ukiitazama hiyo mistari utaona tunafundishwa hapo kuwa, kuhani yeye mwenyewe anapomwendea Mungu inatakiwa atubie kwanza uovu wake. Kama anatakiwa atubue uovu wake maana yake anao.

Unaposoma maandiko ni kuhani wetu mkuu Bwana Yesu Kristo peke yake ndiye ambaye hakuwa na hatakuwa na dhambi. (Hakufanya ingawa alichukua dhambi za ulimwengu)

Katika kipindi cha kuutafuta uso wa Mungu makuhani lazima tujihadhari na mtazamo wa moyoni wa kujihesabia haki kama hao wengine woote tuwaonao wakikumbwa na hili tatizo kama ni wadhambi mnoooo kuliko sisi. MWENYE MASIKIO NA ASIKIE!!!!!

Ondoa moyoni mwako wazo kuwa Mungu atakusikia kwa sababu wewe ni mwenye matendo mema kuliko wengine, hapana. Mungu atakusikia kwa sababu kuu moja tu: umeona kosa lako wewe na hao wengine woote na umeamua kuliungama na kujutia. Ndiyo maana ya unyenyekevu.

Ngoja nikupe mfano huu uone hiki ninachotaka nikutazamishe Angalia Danieli alivyomwendea Mungu katika kipindi ambacho aliwakasirikia wana wa Israeli. 

“Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo; katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako; wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi. Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa. Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi. Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi; wala hatukuitii sauti ya BWANA, Mungu wetu, kwa kwenda katika sheria zake, alizoziweka mbele yetu kwa kinywa cha watumishi wake, manabii. Naam, Israeli wote wameihalifu sheria yako, kwa kugeuka upande, wasiisikilize sauti yako; basi kwa hiyo laana imemwagwa juu yetu, na uapo ule ulioandikwa katika sheria ya Musa, mtumishi wa Mungu; kwa sababu tumemtenda dhambi.” (Danieli 9:1-11)

Ukiisoma hiyo mistari kumi na moja utagundua Danieli alikuwa anautafuta uso wa Mungu ili Mungu awaondolee adhabu ambayo aliwapelekea kwa sababu walimkasirisha. Aliwapeleka utumwani.

Danieli anaposimama ili azungumze na Mungu, kwanza alijua kabisa kuwa kisa cha tatizo wanalopitia ni dhambi, na alijua kabisa kuwa wanapitia adhabu kali sana.

Alipokuwa anaziungama dhambi mbele za Mungu, Danieli hakujihesabia haki kabisaa.

Sikiliza anasema hivi: “Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; tumefanya dhambi, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na hukumu zako;wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii,”

Sikiliza kwa makini hayo maombi. Hasemi Wamefanya dhambi, hawajaisikiliza sauti ya watumishi wako, n.k. Anasema TUMEFANYA DHAMBI!!!!

Angalia kitu cha ajabu hapo, Danieli ni mtumishi wa Mungu kabisaa yeye ni nabii, angalia anasema hatukuwasikiliza watumishi wako. Anapotubu na kuungama anajihesabu yeye na hao wana wa Israeli ni wakosaji, ingawa kwa kweli utaona yeye huenda hakuifanya hiyo dhambi.

Sikiliza Bwana Yesu Kristo kama kuhani mkuu, aliichukua dhambi ya ulimwengu, unajua maana ya kuuichukua dhambi ya ulimwengu? Maana yake ni hii yeye alijitwisha hiyo dhambi kama ni yeye amefanya, ndiyo maana ya kuchukua dhambi ya ulimwengu.

Kwa maana nzuri maombi yake alisema vivyo hivyo kama alivyosema Danieli. Tumekutenda dhambi, n.k!!! Hakuwa na mtazamo kama huu wa kusema wamefanya dhambi …..

Ngoja nikuambie kitu; unapoiombea nchi yako ya Tanzania ili Mungu aiokoe katika majanga ya namna hii, unajua ni rahisi sana mpendwa ukiwa humu ndani ya nchi hii ukaona kama hao watu wa nchi za Ulaya, China, Amerika, Uarabuni n.k kama ni watu waovu kweli.

Ni rahisi kuona aisee Wachina bwana hawana Mungu wale ndiyo maana Mungu anawachapa kwa tauni hii ya Corona, ni rahisi kufikiri wazungu bwana wako tofauti na sisi Waafrika, wamemwacha Mungu, ndiyo maana ameamua kuwachapa. n.k.

Sikiliza mpendwa ukitaka leo hii kuwa kuhani wa ulimwengu yaani ukasimama mahali palipoharibika ulimwenguni jifunze kuomba maombi ya mfumo wa kutokuwaona hao ni waovu.

Ukisikia vita sehemu nchi fulani usifikiri Watanzania ni watu watakatifu kuliko hao wa taifa hilo. Au ukisikia nzinge na tauni inazipiga nchi fulani usifikiri sisi huku ni bora kuliko hao. Unapokwenda kuomba ulinzi kwa Mungu tubu mpendwa bila kujiona wewe ni bora.

Mimi naamini sisi Watanzania tutaokolewa tu kwa maombi ya toba na unyenyekevu. Si kwa sababu eti tuna Mungu.

Ngoja nikuulize swali wewe usemaye unajua hao wazungu walimwacha Mungu n.k. hivi kweli sisi Waafrika tuna Mungu? Hivi sisi Waafrika hatuna maovu? Wewe angalia namna tunavyoabudu miungu, angalia uzinzi, angalia uchawi, angalia namna wanaume wasivyowatunza wake zao na watoto.

Mungu anasema  hivi: “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.” (1 Timotheo 5:8)

Maana yake Mkristo wa sifa hiyo hana tofauti na mpagani aliyesema hakuna Mungu.

Angalia nchi hii ilivyo na damu za watu wengi tu katika ardhi. Watu wengi hutoa mimba na kuua katika nchi hii nakuambia. Nchi hii ndiyo unasikia watu wanaua wanadamu wenzao wenye ulemavu wa ngozi ili tu wapate mali au ukuu, n.k.

Nchi hii ina watu wengi mnooo wanaoamini ushirikina, n.k. mtu haolewi mpaka akaloge, akiolewa analoga ili mume akae naye.

Nenda kanisani uone dhambi zipo nje nje, si watumishi na waaminio kila siku unaona na kusikia wameanguka na hata kuwa waongo angalia watu wengi mnoo wamejeruhiwa na kuumizwa mno na sisi watumishi katika nchi hii n.k.

Angalia dhambi ya uongo na udanganyifu n.k. Mimi nimejaliwa kutembea nchini humo, aisee nchi hii ina makahaba wengi mnoo na wengine wako makanisani kabisaa.

Angalia humo makanisani namna tupatavyo viongozi, wewe angalia namna nchi hii tunavyopata viongozi n.k. Wengi hutoa rushwa n.k.

Angalia kanisani namna tunavyoiba fedha na sadaka ya Mungu n.k. Umewahi ona mradi wa kanisa unaenda?

Angalia wivu na husuda na kudhulumu wajane na mayatima nchini humu tulivyo.

Angalia dhambi ya uvivu na kutolipa kodi sijakosea nasema kodi jinsi tulivyo.

Angalia namna tunavyoiba hiyo kodi ya serikali jinsi tulivyo. Angalia dhambi ya ulevi jinsi ilivyo nchini mwetu.

Kwa haya tu ninayokuambia unaweza ukaniambia sisi tupo salama kuliko hao wanaokufa huko na Corona? Na nchi zao kuliwa na nzige n.k?

Sikilizeni makuhani hebu tuondoe hayo mawazo ya kitoto kuwa sisi tuna haki kama taifa kuliko mataifa mengine.

Wengine wanasema unajua sisi Waafrika mafua hayatatudhuru. Sikia ni tauni. Kama tusipomwomba Mungu kwa unyenyekevu mafua tunayofikiri tutayamudu; yatatumudu nawaambia.

Katika kipindi kama hicho tusijiangalie tulivyo TUNAHITAJI TUMRUDIE MUNGU KWA KILIO BILA KUJIHESABIA HAKI. TUKUBALI KUWA TUMEMKOSEA MUNGU NA ANA HAKI KABISAA YA KUTURUDI. KINACHOTAKIWA TUKIFANYE TUSIJIONE NI WENYE HAKI.

Hatuna haki tuungane makuhani tumwambie BWANA TUMEKUFANYIA DHAMBI.

Danieli naamini hakufanya hayo maovu lakini alilijua hili ninalokuambia alisema tumekufanyia dhambi sisi na Israeli woote!!

Ukiwa ni mtu wa tabia hii, Mungu ni rahisi kukuokoa wewe na nyumba yako. Mungu alimsikia Danieli na makuhani wengine, fahamu hata wewe na mimi atatusikia tu. Hebu chukua hii na uanze kuliweka kwenye matendo.

Tuonane katika katika salamu za mwezi ujao.

Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo;
1. App yetu ya huduma yenye jina  “HUSONEMU (MWAKATWILA)” utaipata Play Store kwenye link pale juu, ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

2. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

3. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

4. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya Facebook (f) "like" na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

5. Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila

6. DVDs 📀 au CDs 💿

7. VITABU.

NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

8. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

9. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:- radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 754 849 924 Au
+255 756 715 222

Wako
Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

Salamu – Machi, 2020

Salamu – Machi, 2020

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Ndugu yangu naamini unaendelea vema. Mwezi uliopita yaani wa pili nchi yetu imetangaza rasmi kuhusu ugonjwa wa Corona.

Kumbuka salamu hizi ndani yake zimebeba maarifa ya nini ufanye ikiwa mtu utakutana na tauni kama hizi. Fanyia kazi yale Mungu atakufundisha katika somo hili.

Mwezi uliopita tumekuwa na semina nyingi sana. Tumekuwa na semina iliyochukua wiki karibu mbili katika kanisa la KKKT Bethel. Tulikuwa na semina ilikuwa inaanza saa kumi na moja mpaka saa moja yaani Morning glory

Pia tulikuwa na kongamano la maombi pale KKKT Mjini ilikuwa ni kongamano la wiki mzima. Lilikuwa kongamano zuri. Pia tulipata nafasi ya kufundisha ibada mbili pale katika kanisa la Moravian Luanda.

Tunamshukuru Mungu kwa ajili ya maombi yenu. Pia nikuhimize ombea sana taifa letu madhara ya Corona yasitupate. Usikae kimya omba. Kumbuka tuna salamu zenye kichwa

MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU (ENEO LA KUOKOLEWA KATIKA KIPINDI CHA MAJANGA ULIMWENGUNI)

Hebu tusogee mbele kidogo.

Katika salamu zilizopita tulijifunza jambo la tatu nalo lilikuwa LAZIMA UOMBE KWA MFUMO WA MAOMBI YA KUUTAFUTA USO WA MUNGU.

Katika salamu za mwezi huu wa tatu nataka tuendelee mbele kidogo kwenye eneo hilo hilo.

MUNGU HUWA ANA TABIA YA KUUFICHA USO WAKE

Angalia tena mistari hii: “BWANA akamtokea Sulemani usiku, akamwambia, Nimesikia uliyoyaomba, na mahali hapa nimejichagulia kuwa nyumba ya dhabihu. Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.” (2 Mambo ya Nyakati 7: 12-15)

Ukiipitia hiyo mistari utaona Mungu anasema “….Watajinyenyekesha, na kuomba na kunitafuta uso …..” Ukisikia neno tafuta maana yake hakipo, kimepotea, au hakionekani au ni kazi kubwa kukiona, n.k.

Kwa nini Mungu katika kipindi hicho ambacho anasema akipeleka tauni inatakiwa watu walioitwa kwa jina lake waombe na wamtafute uso wake?

Uso wake unakuwa umekwenda wapi? Na kwa nini kipindi hicho watu wake walioitwa kwa jina lake waingie gharama ya kuutafuta uso wake? Kwa nini ajifiche? Mungu hawezi kusema mnitafute kama hajajitenga na hao watu.

Sikiliza, sababu inayomfanya Mungu aufiche uso wake katika kipindi hicho inakuwa ni kwasababu ya hasira yake

Sikiliza, Mungu huwa anakasirika sana tu, na pia huwa anafurahi sana tu n.k.

Hasira zake hutokea anapoona dhambi za wanadamu zimezidi kiwango, hapo ndipo hukasirika sana. Na akikasirika ana tabia ya kuachilia adhabu na anapoachilia adhabu huwa ana tabia kuuficha uso wake kwa sababu nyingi tu.

Moja ya sababu ya kuuficha uso wake ni hii, ILI ASISIKIE KILIO CHA HAO WATU!!!! Kwa maana nzuri ndani yake huwa anakuwa na hasira kali.

Mungu anapofurahia watu wake huzungumza nao uso kwa uso na haufichi uso wake. Na apouleta uso wake maana yake watu hao hukaa nuruni ambako ulinzi wao huwa ni mkubwa mno.

Mungu anapo wafurahia watu wake uso wake anauleta au haufichi, Angalia mistari hii uone hiki ninachokuambia: “Naye BWANA akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.” (Kutoka 33:11)

Mungu alizungumza hapo na Musa uso kwa uso kabisaa kama rafiki yake. Angalia mistari hii mingine utaona kitu cha kujifunza katika eneo ambalo anasema wakiutafuta uso wake.

“BWANA akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii; nami nitamtuma malaika aende mbele yako; nami nitawafukuza Mkanaani, na Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi; waifikilie nchi imiminikayo maziwa na asali; kwa maana mimi sitakwenda kati yenu; kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu; nisiwaangamize ninyi katika njia. Watu waliposikia habari hizo mbaya wakaomboleza wala hapana mtu aliyevaa vyombo vyake vya uzuri. BWANA akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli, Ninyi ni watu wenye shingo ngumu; kama mimi nikiingia kati yenu dakika moja, nitawaangamiza; basi sasa vueni vyombo vyenu vya uzuri ili nipate kujua nitakalowatenda. …….Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako. Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha. Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa. Kwa maana itajulikanaje kuwa nimepata neema mbele zako, mimi na watu wako? Siyo kwa sababu unakwenda pamoja nasi, hata mimi na watu wako tutengwe na watu wote walio juu ya uso wa nchi? BWANA akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako.” (Kutoka 33:1-5 na 13-17)

Ukiipitia hiyo mistari utaona Mungu alipowakasirikia wana wa Israeli aliuficha uso wake. Alisema akiingia kati yao au akiuleta uso wake kwa sababu ya dhambi zao atawaangamiza dakika moja.

Sikiliza, Mungu anapokasirika na kuachia adhabu fahamu anakuwa ameuficha uso wake. Kipindi hicho usifikiri utakutana naye kama ulivyokuwa unakutana naye zamani.

Ngoja nikupe mfano. Mungu alipowakasirikia wana wa Israeli baada ya kuabudu sanamu, Musa alikaa mlimani akiutafuta uso wa Mungu kwa muda wa siku arobaini.

Fikiria siku ya arobaini ndipo akauonyesha uso wake na kumwambia Musa amekubali.

Kwa lugha nzuri siku zote hizo thelathini na tisa Mungu aliuficha uso wake.

Ngoja nikupe mfano mwingine. Unakumbuka Bwana wetu Yesu Kristo alipoichukua tu dhambi ya ulimwengu Mungu aliyekuwa pamoja naye siku zote aliuficha uso wake?

Bwana Yesu Kristo alijua ndiyo maana alilia “Baba mbona umeniacha?” Uso wake Mungu ulifichwa, dunia yote ikawa giza, muda wa masaa matatu hivi. Alipourudisha uso wake nchi ikapata nuru tena.

Mungu anapouficha uso wake fahamu giza hutawala, hapo ndipo wanadamu hukutana na magumu kutoka ulimwengu wa giza kwa kiwango cha juu mno.

Sikiliza nikuambie. Uso wa Mungu unapotutazama humu ulimwenguni ulinzi wa ulimwengu na kila kitu huwa mkubwa. Mimi nakuambia Mungu akificha uso wake ambao ni nuru kwa ulimwengu watu waishio humo ulimwenguni hujikuta kwenye misiba ya kila aina.

Uso wake unapokwenda nasi fahamu anatuona na anatuhurumia mnooo na kutuokoa na maradhi nk. Sasa Anapokasirika na kuachilia tauni ulimwenguni au nzige n.k. ana tabia ya kuuficha uso wake ili asiwaone wanadamu wanavyoteseka. Ili akawaokoe. KWA SABABU ANA HURUMA SANA!!!

Mungu ana akili nyingi mnoo anajua akituangalia tu atatuonea huruma kwa hiyo hukimbilia kuuficha uso wake ili asiangalie.

Umewahi kufikiri siku ile ya Sodoma na Gomora kwa nini hakwenda kule? Unaweza kuniuliza kivipi. Sikiliza maneno haya: “BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua. Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za BWANA. Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? …..Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi. Basi BWANA alipokwisha kuzungumza na Ibrahimu, akaenda zake; Ibrahimu naye akarudi mahali pake….” (Mwanzo 18:20-23 na 32)

Angalia na hii mistari uone ninachokuambia: “Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi.” (Kutoka 19:1)

Ukiipitia hiyo mistari utaona Mungu alipomfuata Ibrahimu hakuwa peke yake, alikuwa na malaika wawili. Mungu alibaki na Ibrahimu akiongea naye kwa ajili ya Sodoma na Gomora, wale malaika wawili wakawaacha wakiongea.

Mungu alipomaliza mazungumzo na Ibrahimu aliondoka. Biblia haisemi alienda Sodoma na Gomora. Walioingia Sodoma na Gomora ni malaika wawili. Jiulize Mungu alienda wapi?

Mimi naamini alirudi mbinguni na alienda kuuficha uso wake. Kwani alichokitarajia kukipata kutoka kwa Ibrahimu alikikosa, nacho kilikuwa ni utetezi. Ibrahimu hakufanya toba iliyoshiba kwa ajili ya watu wa Sodoma na Gomora kama Musa alivyofanya kwa ajili ya wana wa Israeli.

Malaika walichoma Sodoma na Gomora kilio chao hakikusikika kwa sababu Mungu aliuficha uso wake asione.

Mungu hapendi kututesa au kutuua: “Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.” (Maombolezo ya Yeremia 3:31-33)

Mungu ukiona ameamua kuachia tauni fahamu hata uso wake huuficha kwa sababu hapendi kuona wanadamu wakiteseka.

Mungu ni Baba yetu, ndiye aliyetuumba, kama mzazi yeyote yule mwenye uungwana ana tabia ya kuwachapa au kuwapiga watoto wake ili wawe na adabu.

Unajua watu wengi hawajui kuwa Mungu anapiga. Angalia mistari hii: “Basi hivi karibu nitamwaga ghadhabu yangu juu yako, nitazitimiza hasira zangu juu yako, nami nitakuhukumu sawasawa na njia zako; nami nitakupatiliza machukizo yako yote. Jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; nitakupatiliza njia zako na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako; nanyi mtajua ya kuwa mimi, BWANA, napiga.” (Ezekieli 7:8-9)

Umesikia maneno hayo mpendwa? Anasema “nanyi mtajua ya kuwa mimi, BWANA, napiga.” Mungu akikasirika anapiga tena anapiga kweli. Unaweza kusema haiwezekani bwana!!

Umewahi kufikiria hivi. Kama Mungu huyu alimwua mtoto wake wa kwanza ampendaye sana yaani Bwana Yesu Kristo ili amwokoe mwanadamu?

Kama aliweza kuua mtoto wake mpendwa asiye na dhambi kwa ajili ya wenye dhambi unafikiri itakuwa shida kuwaua hao wanadamu halafu wenye dhambi na jeuri na ukorofi?

Mimi nawaambia ukweli Mungu anaweza kabisa kuruhusu tauni na akauficha uso wake kabisaa ili dawa au adhabu iwaingie vizuri wanadamu!!!!

Angalia mistari hii, tena ipo katika agano jipya: “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake. Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.” (Waebrania 12:5-11)

Mungu anaweza kabisa kuturudi sisi watoto wake. Fikiria wasio watoto wake itakuwaje? Kumbuka watoto wake tu huturudi ili tuwe na adabu fikiria watu wake waliomo ulimwenguni je!

Kama anaweza kupiga kuanzia madhabahuni huko nje itakuwaje? Hebu tuliangalie pia jambo la Nne

JAMBO LA NNE: JIFUNZE KUUTAFUTA USO WAKE KWA TOBA NENDA KWA KUTUMIA NAFASI YA UKUHANI TU.

Sikiliza Mungu anapokuwa katika hali ya namna hii lazima wamwombao wabadili mfumo wa maombi yao, inatakiwa waanze kuomba maombi ya toba tu.

Pia fahamu ili Mungu asikie huko aliko katika kipindi kama hicho atawasikia makuhani tu.

Kwa sababu kuhani ni mpatanishi, au kwa lugha nzuri ni mwombezi. Kuhani si mchungaji, au nabii, au mwalimu, au mtume. Mungu akikasirika na kuuficha uso wake ni kuhani peke yake anaweza kumsikiliza.

Kipindi hicho hasikilizagi nabii, mwalimu, mchungaji, mwinjilisti au mtume. Ngoja nikupe mfano uone: “Musa akamwambia Haruni, Haya, shika chetezo chako, ukatie moto ndani yake, moto wa madhabahuni, kisha utie na uvumba juu ya moto, ukakichukue haraka, wende nacho katika huo mkutano, ukawafanyie upatanisho; kwa kuwa ghadhabu zimetoka kwa BWANA; hiyo tauni imeanza. Basi Haruni akakishika chetezo kama Musa alivyonena, akapiga mbio akaenda katikati ya mkutano; na tazama, tauni ilikuwa imeanza kati ya watu; akatia uvumba juu ya moto na kufanya upatanisho kwa ajili ya hao watu. Akasimama kati ya hao waliokufa na hao waliokuwa wakali hai; tauni ikazuiwa. Basi waliokufa kwa tauni walikuwa kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya hao waliokufa katika jambo la Kora. Haruni akamrudia Musa pale mlangoni pa hema ya kukutania; hiyo tauni ikazuiwa.” (Hesabu 16:46-50)

Ukiipitia hiyo mistari utaona hiki ninachokuambia. Musa ni nabii hakugusa chetezo wala hakuingia katika huduma ya kufanya upatanisho.

Huduma hiyo ya upatanisho aliifanya kuhani tu. Mungu anapoleta tauni na tauni ikaanza kuua watu fahamu uso wake anakuwa ameuficha. Wanaoweza kumbembeleza na uso wake ukaonekana ni makuhani peke yao.

Hapo hakuna wafalme, wakuu, manabii au walimu, au waimbaji, au wainjilisti au mitumie. Atawasikiliza makuhani peke yao.

Sikiliza makuhani leo hii ni kanisa, unaweza kuwa mchungaji au askofu au mwalimu au padri au mwinjilisti au mtume au nabii lakini usiwe kuhani.

Katika agano jipya kuhani ni mtu yeyote aliyenunuliwa kwa damu ya Bwana Yesu Kristo

“Tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina.” (Ufunuo 1:5-6)

Angalia na mistari: “Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.” (Ufunuo 5:9-10)

Kila aliyenunuliwa kwa hiyo damu ni kuhani. Sikiliza makuhani, wewe ndiwe pekee umewekewa kazi hii ya kufanya maombezi yaliyobeba toba iletayo upatanisho ili Mungu aturehemu na tauni izuiliwe.

 Kanisa tusipojitambua katika kipindi na sisi tukakaa kama watu wengine nawaambia ukweli uso wa Mungu utakuwa mbali; ataendelea kuuficha tu na tauni haitazuiliwa ulimwenguni.

Angalia mistari hii uone hiki ninachokuambia: “Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake. Hao makuhani, wahudumu wa BWANA, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee BWANA, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao? Hapo ndipo BWANA alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake. BWANA akajibu, akawaambia watu wake; Tazameni, nitawaletea nafaka, na divai, na mafuta, nanyi mtashiba kwa vitu hivyo; wala sitawafanya tena kuwa aibu kati ya mataifa; lakini jeshi lililotoka kaskazini nitaliondolea mbali nanyi, nami nitalifukuza mpaka nchi ya ukame na ukiwa; sehemu yake iliyo mbele itaingia katika bahari ya mashariki, na sehemu yake iliyo nyuma itaingia katika bahari ya magharibi; na uvundo wake utapanda juu, na harufu yake mbaya itapanda juu, kwa sababu ametenda mambo makubwa.” (Yoeli 2:17-20)

Ukiipitia hiyo mistari utaona Mungu aliuficha uso wake ili awaadhibu wanadamu. Alichokifanya ili aone yaani uso wake urudi kuwatazama hao watu, aliagiza makuhani walie au wakamtafute.

Hakusema manabii, n.k. Alisema makuhani. Sikilizeni kanisa, MUNGU ANAWASUBIRI NINYI MLIE. Bahati mbaya kipindi kama hiki akili ya kanisa inakuwa kwa viongozi wa nchi, au kwa maaskofu au kwa manabii, n.k.

Sikiliza wewe kuhani yaani wewe uliyenunuliwa kwa damu ya Bwana Yesu Kristo unaweza ukawa askofu, kiongozi fulani au mchungaji, mwinjilisti na inawezekana kabisa usiwe kiongozi au nabii au mwinjilisti, n.k. ANZA KUUTAFUTA USO WA MUNGU KWA TOBA UONAPO TAUNI AU NZIGE NK VIMEPELEKWA ULIMWENGUNI NA MUNGU.

Utafute uso wa Mungu, ingia gharama, kwa ajili ya watu wako, nchi yako, taifa lako, na ulimwengu woote.

Tubia maovu au dhambi au makosa ya aina yoyote ambayo ndiyo chanzo cha hasira kutoka kwa Mungu.

Jifunze KULIA, SI KUKEMEA TUUUU MPENDWA; KUHANI LIA MBELE ZAKE MUNGU NDIPO USO WAKE UTAONEKANA NA TAUNI AU NZINGE AU MAJANGA YOYOTE KAMA CORONA N.K ZITAZUIWA KWA MAARIFA ATAKAYOYAACHILIA.

Au kama tauni imepelekwa, Mungu akiuleta uso wake fahamu atawaokoa wale waliao kwa ajili ya uovu utendwao katika mji wao au taifa lao au nyumba yao.

Nataka kukutia moyo usijidharau wewe kuhani ndiwe pekee mwenye kuurejesha uso wa Mungu ili uende na watu walioko duniani.

Unaweza kumshirikisha mpendwa mwingine ujumbe huu.

Tuonane mwezi ujao katika kona hii ya salamu za mwezi. BARIKIWA

Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo;
1. App yetu ya huduma yenye jina  “HUSONEMU (MWAKATWILA)” utaipata Play Store kwenye link pale juu, ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

2. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

3. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

4. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya Facebook (f) "like" na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

5. Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila

6. DVDs 📀 au CDs 💿

7. VITABU.

NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

8. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

9. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:- radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 754 849 924 Au
+255 756 715 222

Wako
Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.