1⃣4⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE KUISHINDA DHAMBI YA UZINZI
Na: MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA
FUATANA NASI:- APP, FACEBOOK, INSTAGRAM, ONLINE RADIO 📻, WHATSAPP, WEBSITE & YOUTUBE, Kwa links zilizoko kwenye HII LINK hapa:
KUPATA APP YETU “HUSONEMU (MWAKATWILA) APP” BONYEZA LINK HII HAPA:
🗓 02 Februari, 2019
Bwana Yesu Kristo asifiwe sana sana. Nimeupata muda huu nimeona niutumie kukuletea mwendelezo wa somo hili la namna unavyotakiwa ufanye ili upate kuishinda dhambi ya uzinzi.
Hebu tusogee mbele kidogo tujifunze kitu kingine muhimu ambacho kinaweza kuwa chanzo cha tabia ya uzinzi.
CHANZO CHA PILI CHA TABIA YA UZINZI NI TABIA INAYOTOKANA NA ROHO AU (PEPO)
Baada ya kujifunza eneo hilo la tabia ya uzinzi inayotokana na mwili natamani nikuonyeshe pia chanzo kingine kinachoweza kuwa ndiyo kiini cha tabia ya uzinzi.
Mtu anaweza kuwa na tabia fulani mbaya ambayo chanzo chake ni roho au mapepo yaliyoimiliki roho ya huyo mtu na mwili wake na hata moyo wake. Yaani mfumo woote wa akili.
Angalizo, si kila mtu mwenye tabia ya uzinzi basi ana pepo la uzinzi. Watu wengi wanaosumbuliwa na tabia ya uzinzi wanahisi sana kuwa wana roho ya uzinzi.
Sikiliza ninaposema roho ya uzinzi simaanishi roho yako wewe. Fahamu Mungu alipokuumba alikuumba wewe kwa mfano wake ambao ni roho.
Mungu ni Roho, maandiko yanasema hivi. “Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.” (Yohana 4:24)
Mungu ni Roho alikuumba wewe kwa mfano wake ambao ni roho, anaposema imetupasa kumwabudu katika roho fahamu anaizungumzia roho yako wewe ndiyo inatakiwa imwabudu yeye.
Kumbuka tulikotoka ulipewa mwili. Yaani wewe uliye roho ulipewa mwili ukapewa na nafsi au moyo. Ili wewe uliye roho upate kuishi kwenye ulimwengu huu ulipewa mwili.
Mwili ndiyo unatupa nafasi ya sisi tulio roho kuishi humu duniani. Au katika ulimwengu huu unaoonekana. Roho ikitengana na mwili roho hiyo haiwezi kuishi katika huu ulimwengu unaoonekana.
Unaweza kujiuliza inaenda wapi? Hapo ni somo lingine kabisa na ni pana mno. Si kila mtu ambaye roho yake imetengana na mwili au kufa roho yake inakwenda mbinguni.
Soma Biblia kwa kutulia utagundua vitu vya ajabu sana. Wengine roho zao zinabanwa na wanadamu (wachawi) zikitumikishwa mahali.
Biblia inasema hivi “Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena; bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari; na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu. Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe. Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza,” (Ufunuo 18:11-15)
Ukiipitia hiyo mistari utaona hapo kuna biashara ya roho za watu. Angalia kwa kutulia utaiona hapo biashara ya ROHO NA MIILI YA WATU.
Biashara hiyo au hizo walizipata Babeli yaani kwenye ufalme wa giza. Ni biashara kabisa kama vile biashara ya magari, nk. Kuna vitu Mungu akiamua kukufundisha na kukuonyesha vinatisha sana.
Kuna siku Mungu alinionyesha mambo haya niliogopa sana sana. Umewahi kujiuliza swali kwa nini Bwana Yesu Kristo alisema fufueni wafu? Ukilitazama hilo neno kitoto huwezi kumwelewa, mimi nakuambia ukweli kuna watu wengi sana roho zao ziko masokoni zikiuzwa kwa wafanyabiashara ili wazitumie kuwaingizia mali kuwalimia nk.
Roho zingine zimebanwa na mauti na zingine zimebanwa baharini, zingine zimebanwa kuzimu.
Angalia mistari hii. “Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu...... Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:5-6 na 12-15)
Ukiipitia hiyo mistari utagundua hayo ninayokuambia. Ni somo refu sana nilitaka tu nikuonyeshe kuhusu roho ilipewa mwili ili iishi katika ulimwengu huu.
Inapoachana na mwili inaweza kwenda wapi. Sikiliza NJE YA BWANA YESU KRISTO NAWAAMBIA UKWELI ROHO YA MTU INAPOACHANA NA HUU MWILI ITAKWENDA KWENYE MOJA YA MAENEO HAYO HAPO.
Nakusihi na kukushauri sana mwamini Bwana Yesu Kristo mapema kabla haujakutana na haya ninayokufundisha. Mpokee Bwana Yesu Kristo ili akuandike kwenye kitabu chake cha uzima. Mimi nakuambia ukweli kuna kitabu cha majina yanayoandikwa mbinguni, mtu au roho ya mtu aliyeandikwa humo ndiyo inaitwa ina uhai.
Siku inapotengana na mwili inavushwa kwenye hayo maeneo TATA AU MABAYA. Haibanwi na mauti kama wasiojua wengi wasemavyo kila nafsi itaonja mauti.
Sikiliza Roho yako inavyotolewa kwenye mwili inaondoka na nafsi yake yaani pumzi hai ya Mungu. Sikiliza, roho yako inapotolewa katika mwili inakuwa na ufahamu kabisaa inajua inafahamu kila kitu yaani inakuwa na akili ila inakosa mwili huu wa nyama tu.
Yaani unajua kabisaa kuwa umekufa na unajua kabisaa huna Yesu na unaenda kubaya au kuzuri. Ninachotaka nikufundishe ni hivi si wote wanaonja au wanabanwa na mauti. Mtu au roho iliyo na Bwana Yesu Kristo inapita mautini.
Biblia inasema hivi “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.” (Yohana 5:24).
Nje ya huyu BWANA YESU KRISTO huwezi kupita hapo utabanwa tu au utaonja hiyo mauti nakuambia. Watu wengi bahati mbaya wanamdharau sana Bwana Yesu Kristo, hawataki kulisikia neno lake ili wamwamini wameshikilia watu wengine. SIKILIZA NIKUAMBIE HAKUNA MTU MWINGINE NJE YA BWANA YESU KRISTO ANAYEWEZA KUKUVUSHA HAPO AU HUKO KWENYE YALE MAENEO MENGINE ROHO ZA WATU ZILIKOBANWA.
Ninawaona watu wengi sana wanamwacha Bwana Yesu Kristo na kisa eti wanaolewa au kazi au kupata mitaji na kuanza kuwa na imani nyingine nje ya Bwana Yesu Kristo.
Huwa nasikitika sana sana. Ungejua ungevikosa hivyo vyote ili umpate huyu Bwana Yesu Kristo ili akuvushe kwenye hayo maeneo na akupe wewe uliye roho pumziko au uhai.
Simhukumu mtu ila nasikitika kwa kuwa yanafichwa hayo machoni pako.
Ngoja nirudi kwenye pointi yangu. Roho iliumbwa ikae kwenye mwili, fahamu mwili wa mtu uliumbwa ili ukalishe roho. Sasa sikia hata Mungu ambaye ni Roho anaweza kukaa ndani ya huo mwili.
Sikia, pia mwili huo wa mtu unaweza kukalisha hata roho zingine kabisa zaidi ya roho ya huyo mtu mwenye mwili au Roho ya Mungu au roho zingine mbaya tunaita mapepo.
Angalia mfano huu “Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia.” (Luka 8:30)
Unaposoma hiyo mistari unaona namna mwili wa mwanadamu unavyoweza kuzihifadhi au kukaliwa na roho nyingi sana zaidi ya roho yake huyo mtu.
Ngoja nikupe mfano huu. Hebu chukulia mfano wa nyumba tu hizi tunazoishi. Utaona nyumba inajengwa na mwenye nyumba na huyo mwenye nyumba anao uwezo wa kuishi ndani ya hiyo nyumba au kuingia na kutoka ndani ya hiyo nyumba.
Mtu anaweza kumjengea mwanawe nyumba ili amweke mwanawe ndani ya hiyo nyumba na akampa kabisa hiyo nyumba. Lakini mzazi anapomjengea mwanawe nyumba haimanishi huyo mzazi hana uhalali wa kuingia ndani ya hiyo nyumba.
Pia huyo mtoto anaweza kuingiza kila mtu amtakaye kwenye hiyo nyumba aliyojengewa na baba yake. Wanaweza kuingia wema na wabaya kulingana na utaratibu uliowekwa.
Sikiliza hata Mungu alipokuwa anamuumba mtu aliamua kumjengea huyo mtu nyumba. Hiyo nyumba Mungu alipanga aishi huyo mtu na Yeye Mungu kama mjenzi afike hapo katika hiyo nyumba na kuishi na huyo mtu.
Nyumba hiyo ni huo mwili wa mwanadamu. Mungu aliumba nyumba yenye uhai. Si unajua tena Mungu alivyomtalaamu wa mambo, aliumba nyumba ya ajabu iitwayo mwili, nyumba hiyo ina uhai inaweza kukua kutanuka nk.
Uhai huo maandiko yanasema ni damu. Si unajua uhai wa mwili umo ndani ya damu? “Kisha mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli, au miongoni mwa hao wageni wakaao kati yao, atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi. Kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Hapana mtu miongoni mwenu aliye na ruhusa kula damu, wala mgeni aketiye kati yenu asile damu. Mtu ye yote aliye wa wana wa Israeli, au wa hao wageni wakaao kati yenu, ambaye amemshika mnyama, au ndege ambaye huliwa, katika kuwinda kwake; atamwaga damu yake, na kuifunika mchanga. Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila awaye yote atakatiliwa mbali.” (Mambo ya Walawi 17:10-14)
Mpango wa Mungu ilikuwa yeye Mungu ambaye ni Roho aishi humo ndani ya mwili au nyumba yake yeye pamoja na roho ya mtu yaani wewe.
Kilichotokea ni hiki roho yako ilimkataa mjenzi wa hiyo nyumba ambaye ni Mungu. Mungu alipoondoka hapo sasa ndipo balaa likatokea nyumba ikaanza kuvamiwa na roho zingine zinazoitwa mapepo au majini au mizimu nk au shetani mwenyewe.
Unajua dhambi ndiyo inayoitenga roho ya mtu na Roho ya Mungu. Mungu aliweka utaratibu wa namna ya nyumba hiyo itunzwe, alimkataza huyo mtu asile mti wa ujuzi wa mema na mabaya yaani dhambi.
Mtu akala hilo tunda, alipokula tu Mungu akaondoka kwenye hiyo nyumba aliyoijenga na kumweka mtu ili mtu huyo na Mungu waishi pamoja ndani ya hiyo nyumba yaani mwili.
Mtu akajikuta katika hiyo nyumba aliyowekwa na Mungu yaani mwili anavamiwa na roho chafu na kutawaliwa na hizo roho badala ya kutawaliwa na Roho ya Mungu au Roho Mtakatifu.
Ngoja nikuambie kitu hiki. Si watu wote wana mapepo lakini nakuambia ukweli watu wengi sana wana mapep. Unajua ni kwa nini hawajulikani kama wana mapepo?
Ni kwa sababu si kila pepo litamletea ugonjwa au tabia fulani mbaya tu. Mimi nakuambia watu wengi leo hii wanamilikiwa na hayo mapepo kwenye maeneo mengi tu ila hawajui wanaonekana ni watu safi tu kumbe hawako safi.
Pepo linaweza kukaa ndani ya mtu tokea akiwa mtoto na likamtengenezea huyo mtu fursa za kuwa mtu mwenye akili au uwezo fulani mpaka akawa kiongozi mkubwa au mfalme ili tu pepo au shetani amtumie huyo mtu kwa manufaa yake.
Ona mfano huu. “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo. Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule. Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.” (Ufunuo 12:13-17).
Ukiipitia hiyo mistari na kuingia ndani zaidi unaona huyo joka kwenye ulimwengu huu anaonekana alikuwa ni mfalme Herode aliyetaka kumwua mtoto Yesu na mama yake na nchi ya Misri ikawahifadhi.
Fikiria kidogo Herode alizaliwa na baba na mama yake kabisa lakini joka au roho ingine ikamwingia na imwandaa mpaka akawa mfalme ili atumike kuyapitisha hayo joka anayataka.
Kwenye ulimwengu wa roho Mungu alikuwa anamwona shetani au joka akitenda hayo huku duniani kwenye ulimwengu wa mwili tunaona Herode kama mtu akiyatenda hayo.
Mpaka kufikia hapa naona umeanza kupata mwanga wa nini nakuonyesha. Mapepo au shetani anaweza kumwingia mtu mwilini mwake na akayafanya mambo yale shetani anayataka yaani mambo mabaya na huyo mtu huku nje sisi tukamwona ni fulani anayafanya hayo kumbe ni roho mbaya iliyomuingia huyo mtu ndiyo inamwendesha.
Angalia mfano huu uone hiki ninachokufundisha. “Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu. Watu wangu hutaka shauri kwa gongo lao, na fimbo yao huwahubiri mambo; maana roho ya uzinzi imewakosesha, nao wamekwenda kuzini mbali na Mungu wao.” (Hosea 4:11-12).
Hapo kuna neno roho ya uzinzi imewakosesha. Unajua maana yake nini? Sikia Iko hivi: roho au pepo la uzinzi ndilo chanzo cha ukosaji wao. Wewe usome mstari huo kwa uzuri utagundua Mungu anasema alichokiona kikiwakosesha WATU wake ni roho ya uzinzi.
Kumbuka neno mtu ni roho, sasa Mungu anaposema watu wangu wanakoseshwa na roho ya uzinzi maana yake hapo tunatazamishwa hiyo roho kuwa siyo hao watu ila ni roho ya uzinzi au tunaita pepo la uzinzi, kumbuka hayo mapepo ni roho pia.
Sasa yapo mapepo mengi na yamebeba tabia tofauti tofauti. Si kila pepo linamsukuma au kumchochea mtu kwenye tabia ya uzinzi.
Haujawahi kuona watu wenye mapepo au mashetani hayo mashetani yanamkataza asizini. Tena yatamfunga ili hata asiolewe au kuoa?
Sasa sikia unaweza ukajikuta una tabia ya uzinzi ambayo chanzo chake ni hiyo roho tu.
Kuna mtu mmoja ambaye alikuwa na tatizo hili. Yeye alikuwa mkikaa naye hivi ghafla roho hiyo inamwamrisha kuzini tu. Ni mtu mwenye tabia nzuri mpole yaani huwezi mdhania.
Unaambiwa alikuwa akitokewa na hali hiyo hachagui mwanamke, tena alikuwa na uwezo wa ajabu wa kukubaliwa na hao atakaowafuata. Amezini na wabibi, wadada, wasichana wadogo sana yaani ni hatari.
Nilisimuliwa kuwa akiwafuata tu alikuwa wakati mwingine anazini nao kwenye mapagala, kwenye mitaro ya maji machafu, hotelini, chooni, nk yaani haogopi kulifanya hilo tendo popote pale.
Kikichonitisha ni namna alivyokuwa na nguvu ya kuwashawishi wanawake hao aliozini nao ni wengi sana sana. Hiyo roho ikimsukuma asubuhi lazima afanye au mchana au jioni au hata usiku ataamka kutafuta tuuu!!! Fikiria ana mke hapo.
Niliposikia kuwa akitaka mwanamke awe meneja au polisi, mjeshi, nesi mwimba kwaya, mke wa nani, sijui maarufu atamkubalia tu. Nikaelewa sana hilo neno lisemalo roho ya uzinzi imewakosesha.
Sikia, unaweza kujikuta umezini na mtu ambaye hata humkumbuki sura, au mtu ambaye akitokea tena mbele yako utatamani ukimbie yaani ni kituko.
Unajua ni kwa nini? Ni ile roho aliyoibeba ndani yake ndiyo iliyokuvuta ukaanguka.
Mimi ni mtumishi wa Mungu najua haya yote kwa sababu tunakutana na watu kama huyu wengi tu. Unaweza ukawa umeolewa na mwanaume mwema sana tu. Lakini akakutana na dada mwenye roho ya namna hii nakuambia kama mumeo hana nguvu za rohoni ni rahisi mno kujikuta anavutwa na huyo mwanamke na akaanguka naye kabisaa.
Na mumeo akakosa amani miaka yake yoote akijiuliza hivi ilitokeaje. Hata kwa wewe mwanaume ni vivyo hivyo. Unaweza oa mwanamke mzuri sana wa tabia, akikutana na jamaa kama huyo ninayekusimulia na mkeo wewe hutaki asali, hutaki amtumikie Mungu, Mungu ndani yake hayumo unafikiria kitatokea nini?
Nimeishawahi kukutana na wasichana tena wasomi tu wanaomba maombi yaani unamkuta binti anakusimulia tokea amefika chuoni tu hapo ana miaka mitatu kaishatembea kuanzia na wanafunzi wenziwe waalimu wafagiaji hapo chuoni, wajenzi hapo chuoni, wauza mgahawa, wauza duka siyo muuza duka nasema wauza duka, mpishi, nk.
Sitaniii nakuambia ukweli. Anakuambia yeye ndiye anawafuata akimfuata mwanaume tu lazima azini naye.
Ukiwasikikiza watu wa jinsi hiyo ndipo utalielewa Mungu asemavyo hivi. “Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba. Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda. Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu; Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu. Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake. Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.” (Mithali 7:18-27)
Zamani nilikuwa nawalaumu watu wazinzi na ninawahukumu mnoo. Unajua siku Mungu ananifundisha somo hili na kuanza kuona ninapolifundisha somo hili hasa kwa vijana wakike na wakiume nilipoanza kuona mapepo hayo yakilipuka kwa watu wengine na tukiyakemea na hao watu naona wengi wakianguka chini na kuzini na ardhi wengine wakitoa nguo ili wawe uchi ndipo nilipobadilika moyoni mwangu nikaanza kuwaonea huruma watu wenye tabia ya uzinzi hasa wadada.
Wadada wengi adui kawaonea mnoo, kama hujui ni rahisi kuwachukia mno na kuwatengenezea sheria na kila neno baya utawaita na hata kuwaandika nk. Lakini nakuambia ukweli ile roho au mapepo ya uzinzi ndiyo yanawabana na kuwakosesha mnoo.
Hapo nakufundisha elimu kubwa mno. Nikajifunza kwa nini Bwana Yesu alisema watenda dhambi ni watumwa wa dhambi. Sijui wewe hiyo nyumba ya Mungu yaani mwili wako nani anaumiliki? Fikiria mtu ana jeshi humo ndani yake ya mapepo ya uzinzi.
Tofauti yake na huyo Mgerasi ni kuwa huyu amevaa suti na anaendesha gari ni msomi hivi, ni kiongozi hivi, lakini ana mapepo mwilini labda chukulia matatu tu ya uzinzi?
Atajikuta akizini iwe kwenye hiyo gari ukimletea mabinti wa kazi anazini nao, ofisini anazini nao, umpeleke kanisani anazini na mtoto wa mchungaji, nk. Mpaka siku atakapopata ufahamu kuwa hii tabia si ya kawida.
Sasa naona umepata nuru hebu jingalie kama nilivyokuambia nitakuandikia mambo ya kufanya hebu angalia unafikiri huo mwili wako unavyokusumbua je! Ni mwili au ni roho? Kwa ujumla ukiwa na hii roho siyo rahisi kuitawala kama unavyoweza kuutawala mwili.
Ila usiogope uwe wazi tu. Ikiwa unaona hiyo ni roho usifiche niambie tu kuwa naona mimi nimebanwa hii ni roho ya uzinzi.
Naamini umenielewa kwa sehemu hebu tufuatane katika somo hili hapo mbeleni.
Leo nimekuandikia kwa urefu kidogo Mungu akusaidie usome na uelewe na uyafahamu haya.
Mungu akubariki
Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-
Bwana Yesu Kristo asifiwe sana sana. Nimeupata muda huu nimeona niutumie kukuletea mwendelezo wa somo hili la namna unavyotakiwa ufanye ili upate kuishinda dhambi ya uzinzi.
Hebu tusogee mbele kidogo tujifunze kitu kingine muhimu ambacho kinaweza kuwa chanzo cha tabia ya uzinzi.
CHANZO CHA PILI CHA TABIA YA UZINZI NI TABIA INAYOTOKANA NA ROHO AU (PEPO)
Baada ya kujifunza eneo hilo la tabia ya uzinzi inayotokana na mwili natamani nikuonyeshe pia chanzo kingine kinachoweza kuwa ndiyo kiini cha tabia ya uzinzi.
Mtu anaweza kuwa na tabia fulani mbaya ambayo chanzo chake ni roho au mapepo yaliyoimiliki roho ya huyo mtu na mwili wake na hata moyo wake. Yaani mfumo woote wa akili.
Angalizo, si kila mtu mwenye tabia ya uzinzi basi ana pepo la uzinzi. Watu wengi wanaosumbuliwa na tabia ya uzinzi wanahisi sana kuwa wana roho ya uzinzi.
Sikiliza ninaposema roho ya uzinzi simaanishi roho yako wewe. Fahamu Mungu alipokuumba alikuumba wewe kwa mfano wake ambao ni roho.
Mungu ni Roho, maandiko yanasema hivi. “Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.” (Yohana 4:24)
Mungu ni Roho alikuumba wewe kwa mfano wake ambao ni roho, anaposema imetupasa kumwabudu katika roho fahamu anaizungumzia roho yako wewe ndiyo inatakiwa imwabudu yeye.
Kumbuka tulikotoka ulipewa mwili. Yaani wewe uliye roho ulipewa mwili ukapewa na nafsi au moyo. Ili wewe uliye roho upate kuishi kwenye ulimwengu huu ulipewa mwili.
Mwili ndiyo unatupa nafasi ya sisi tulio roho kuishi humu duniani. Au katika ulimwengu huu unaoonekana. Roho ikitengana na mwili roho hiyo haiwezi kuishi katika huu ulimwengu unaoonekana.
Unaweza kujiuliza inaenda wapi? Hapo ni somo lingine kabisa na ni pana mno. Si kila mtu ambaye roho yake imetengana na mwili au kufa roho yake inakwenda mbinguni.
Soma Biblia kwa kutulia utagundua vitu vya ajabu sana. Wengine roho zao zinabanwa na wanadamu (wachawi) zikitumikishwa mahali.
Biblia inasema hivi “Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena; bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari; na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu. Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe. Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza,” (Ufunuo 18:11-15)
Ukiipitia hiyo mistari utaona hapo kuna biashara ya roho za watu. Angalia kwa kutulia utaiona hapo biashara ya ROHO NA MIILI YA WATU.
Biashara hiyo au hizo walizipata Babeli yaani kwenye ufalme wa giza. Ni biashara kabisa kama vile biashara ya magari, nk. Kuna vitu Mungu akiamua kukufundisha na kukuonyesha vinatisha sana.
Kuna siku Mungu alinionyesha mambo haya niliogopa sana sana. Umewahi kujiuliza swali kwa nini Bwana Yesu Kristo alisema fufueni wafu? Ukilitazama hilo neno kitoto huwezi kumwelewa, mimi nakuambia ukweli kuna watu wengi sana roho zao ziko masokoni zikiuzwa kwa wafanyabiashara ili wazitumie kuwaingizia mali kuwalimia nk.
Roho zingine zimebanwa na mauti na zingine zimebanwa baharini, zingine zimebanwa kuzimu.
Angalia mistari hii. “Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu...... Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:5-6 na 12-15)
Ukiipitia hiyo mistari utagundua hayo ninayokuambia. Ni somo refu sana nilitaka tu nikuonyeshe kuhusu roho ilipewa mwili ili iishi katika ulimwengu huu.
Inapoachana na mwili inaweza kwenda wapi. Sikiliza NJE YA BWANA YESU KRISTO NAWAAMBIA UKWELI ROHO YA MTU INAPOACHANA NA HUU MWILI ITAKWENDA KWENYE MOJA YA MAENEO HAYO HAPO.
Nakusihi na kukushauri sana mwamini Bwana Yesu Kristo mapema kabla haujakutana na haya ninayokufundisha. Mpokee Bwana Yesu Kristo ili akuandike kwenye kitabu chake cha uzima. Mimi nakuambia ukweli kuna kitabu cha majina yanayoandikwa mbinguni, mtu au roho ya mtu aliyeandikwa humo ndiyo inaitwa ina uhai.
Siku inapotengana na mwili inavushwa kwenye hayo maeneo TATA AU MABAYA. Haibanwi na mauti kama wasiojua wengi wasemavyo kila nafsi itaonja mauti.
Sikiliza Roho yako inavyotolewa kwenye mwili inaondoka na nafsi yake yaani pumzi hai ya Mungu. Sikiliza, roho yako inapotolewa katika mwili inakuwa na ufahamu kabisaa inajua inafahamu kila kitu yaani inakuwa na akili ila inakosa mwili huu wa nyama tu.
Yaani unajua kabisaa kuwa umekufa na unajua kabisaa huna Yesu na unaenda kubaya au kuzuri. Ninachotaka nikufundishe ni hivi si wote wanaonja au wanabanwa na mauti. Mtu au roho iliyo na Bwana Yesu Kristo inapita mautini.
Biblia inasema hivi “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.” (Yohana 5:24).
Nje ya huyu BWANA YESU KRISTO huwezi kupita hapo utabanwa tu au utaonja hiyo mauti nakuambia. Watu wengi bahati mbaya wanamdharau sana Bwana Yesu Kristo, hawataki kulisikia neno lake ili wamwamini wameshikilia watu wengine. SIKILIZA NIKUAMBIE HAKUNA MTU MWINGINE NJE YA BWANA YESU KRISTO ANAYEWEZA KUKUVUSHA HAPO AU HUKO KWENYE YALE MAENEO MENGINE ROHO ZA WATU ZILIKOBANWA.
Ninawaona watu wengi sana wanamwacha Bwana Yesu Kristo na kisa eti wanaolewa au kazi au kupata mitaji na kuanza kuwa na imani nyingine nje ya Bwana Yesu Kristo.
Huwa nasikitika sana sana. Ungejua ungevikosa hivyo vyote ili umpate huyu Bwana Yesu Kristo ili akuvushe kwenye hayo maeneo na akupe wewe uliye roho pumziko au uhai.
Simhukumu mtu ila nasikitika kwa kuwa yanafichwa hayo machoni pako.
Ngoja nirudi kwenye pointi yangu. Roho iliumbwa ikae kwenye mwili, fahamu mwili wa mtu uliumbwa ili ukalishe roho. Sasa sikia hata Mungu ambaye ni Roho anaweza kukaa ndani ya huo mwili.
Sikia, pia mwili huo wa mtu unaweza kukalisha hata roho zingine kabisa zaidi ya roho ya huyo mtu mwenye mwili au Roho ya Mungu au roho zingine mbaya tunaita mapepo.
Angalia mfano huu “Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia.” (Luka 8:30)
Unaposoma hiyo mistari unaona namna mwili wa mwanadamu unavyoweza kuzihifadhi au kukaliwa na roho nyingi sana zaidi ya roho yake huyo mtu.
Ngoja nikupe mfano huu. Hebu chukulia mfano wa nyumba tu hizi tunazoishi. Utaona nyumba inajengwa na mwenye nyumba na huyo mwenye nyumba anao uwezo wa kuishi ndani ya hiyo nyumba au kuingia na kutoka ndani ya hiyo nyumba.
Mtu anaweza kumjengea mwanawe nyumba ili amweke mwanawe ndani ya hiyo nyumba na akampa kabisa hiyo nyumba. Lakini mzazi anapomjengea mwanawe nyumba haimanishi huyo mzazi hana uhalali wa kuingia ndani ya hiyo nyumba.
Pia huyo mtoto anaweza kuingiza kila mtu amtakaye kwenye hiyo nyumba aliyojengewa na baba yake. Wanaweza kuingia wema na wabaya kulingana na utaratibu uliowekwa.
Sikiliza hata Mungu alipokuwa anamuumba mtu aliamua kumjengea huyo mtu nyumba. Hiyo nyumba Mungu alipanga aishi huyo mtu na Yeye Mungu kama mjenzi afike hapo katika hiyo nyumba na kuishi na huyo mtu.
Nyumba hiyo ni huo mwili wa mwanadamu. Mungu aliumba nyumba yenye uhai. Si unajua tena Mungu alivyomtalaamu wa mambo, aliumba nyumba ya ajabu iitwayo mwili, nyumba hiyo ina uhai inaweza kukua kutanuka nk.
Uhai huo maandiko yanasema ni damu. Si unajua uhai wa mwili umo ndani ya damu? “Kisha mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli, au miongoni mwa hao wageni wakaao kati yao, atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi. Kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Hapana mtu miongoni mwenu aliye na ruhusa kula damu, wala mgeni aketiye kati yenu asile damu. Mtu ye yote aliye wa wana wa Israeli, au wa hao wageni wakaao kati yenu, ambaye amemshika mnyama, au ndege ambaye huliwa, katika kuwinda kwake; atamwaga damu yake, na kuifunika mchanga. Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila awaye yote atakatiliwa mbali.” (Mambo ya Walawi 17:10-14)
Mpango wa Mungu ilikuwa yeye Mungu ambaye ni Roho aishi humo ndani ya mwili au nyumba yake yeye pamoja na roho ya mtu yaani wewe.
Kilichotokea ni hiki roho yako ilimkataa mjenzi wa hiyo nyumba ambaye ni Mungu. Mungu alipoondoka hapo sasa ndipo balaa likatokea nyumba ikaanza kuvamiwa na roho zingine zinazoitwa mapepo au majini au mizimu nk au shetani mwenyewe.
Unajua dhambi ndiyo inayoitenga roho ya mtu na Roho ya Mungu. Mungu aliweka utaratibu wa namna ya nyumba hiyo itunzwe, alimkataza huyo mtu asile mti wa ujuzi wa mema na mabaya yaani dhambi.
Mtu akala hilo tunda, alipokula tu Mungu akaondoka kwenye hiyo nyumba aliyoijenga na kumweka mtu ili mtu huyo na Mungu waishi pamoja ndani ya hiyo nyumba yaani mwili.
Mtu akajikuta katika hiyo nyumba aliyowekwa na Mungu yaani mwili anavamiwa na roho chafu na kutawaliwa na hizo roho badala ya kutawaliwa na Roho ya Mungu au Roho Mtakatifu.
Ngoja nikuambie kitu hiki. Si watu wote wana mapepo lakini nakuambia ukweli watu wengi sana wana mapep. Unajua ni kwa nini hawajulikani kama wana mapepo?
Ni kwa sababu si kila pepo litamletea ugonjwa au tabia fulani mbaya tu. Mimi nakuambia watu wengi leo hii wanamilikiwa na hayo mapepo kwenye maeneo mengi tu ila hawajui wanaonekana ni watu safi tu kumbe hawako safi.
Pepo linaweza kukaa ndani ya mtu tokea akiwa mtoto na likamtengenezea huyo mtu fursa za kuwa mtu mwenye akili au uwezo fulani mpaka akawa kiongozi mkubwa au mfalme ili tu pepo au shetani amtumie huyo mtu kwa manufaa yake.
Ona mfano huu. “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo. Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule. Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.” (Ufunuo 12:13-17).
Ukiipitia hiyo mistari na kuingia ndani zaidi unaona huyo joka kwenye ulimwengu huu anaonekana alikuwa ni mfalme Herode aliyetaka kumwua mtoto Yesu na mama yake na nchi ya Misri ikawahifadhi.
Fikiria kidogo Herode alizaliwa na baba na mama yake kabisa lakini joka au roho ingine ikamwingia na imwandaa mpaka akawa mfalme ili atumike kuyapitisha hayo joka anayataka.
Kwenye ulimwengu wa roho Mungu alikuwa anamwona shetani au joka akitenda hayo huku duniani kwenye ulimwengu wa mwili tunaona Herode kama mtu akiyatenda hayo.
Mpaka kufikia hapa naona umeanza kupata mwanga wa nini nakuonyesha. Mapepo au shetani anaweza kumwingia mtu mwilini mwake na akayafanya mambo yale shetani anayataka yaani mambo mabaya na huyo mtu huku nje sisi tukamwona ni fulani anayafanya hayo kumbe ni roho mbaya iliyomuingia huyo mtu ndiyo inamwendesha.
Angalia mfano huu uone hiki ninachokufundisha. “Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu. Watu wangu hutaka shauri kwa gongo lao, na fimbo yao huwahubiri mambo; maana roho ya uzinzi imewakosesha, nao wamekwenda kuzini mbali na Mungu wao.” (Hosea 4:11-12).
Hapo kuna neno roho ya uzinzi imewakosesha. Unajua maana yake nini? Sikia Iko hivi: roho au pepo la uzinzi ndilo chanzo cha ukosaji wao. Wewe usome mstari huo kwa uzuri utagundua Mungu anasema alichokiona kikiwakosesha WATU wake ni roho ya uzinzi.
Kumbuka neno mtu ni roho, sasa Mungu anaposema watu wangu wanakoseshwa na roho ya uzinzi maana yake hapo tunatazamishwa hiyo roho kuwa siyo hao watu ila ni roho ya uzinzi au tunaita pepo la uzinzi, kumbuka hayo mapepo ni roho pia.
Sasa yapo mapepo mengi na yamebeba tabia tofauti tofauti. Si kila pepo linamsukuma au kumchochea mtu kwenye tabia ya uzinzi.
Haujawahi kuona watu wenye mapepo au mashetani hayo mashetani yanamkataza asizini. Tena yatamfunga ili hata asiolewe au kuoa?
Sasa sikia unaweza ukajikuta una tabia ya uzinzi ambayo chanzo chake ni hiyo roho tu.
Kuna mtu mmoja ambaye alikuwa na tatizo hili. Yeye alikuwa mkikaa naye hivi ghafla roho hiyo inamwamrisha kuzini tu. Ni mtu mwenye tabia nzuri mpole yaani huwezi mdhania.
Unaambiwa alikuwa akitokewa na hali hiyo hachagui mwanamke, tena alikuwa na uwezo wa ajabu wa kukubaliwa na hao atakaowafuata. Amezini na wabibi, wadada, wasichana wadogo sana yaani ni hatari.
Nilisimuliwa kuwa akiwafuata tu alikuwa wakati mwingine anazini nao kwenye mapagala, kwenye mitaro ya maji machafu, hotelini, chooni, nk yaani haogopi kulifanya hilo tendo popote pale.
Kikichonitisha ni namna alivyokuwa na nguvu ya kuwashawishi wanawake hao aliozini nao ni wengi sana sana. Hiyo roho ikimsukuma asubuhi lazima afanye au mchana au jioni au hata usiku ataamka kutafuta tuuu!!! Fikiria ana mke hapo.
Niliposikia kuwa akitaka mwanamke awe meneja au polisi, mjeshi, nesi mwimba kwaya, mke wa nani, sijui maarufu atamkubalia tu. Nikaelewa sana hilo neno lisemalo roho ya uzinzi imewakosesha.
Sikia, unaweza kujikuta umezini na mtu ambaye hata humkumbuki sura, au mtu ambaye akitokea tena mbele yako utatamani ukimbie yaani ni kituko.
Unajua ni kwa nini? Ni ile roho aliyoibeba ndani yake ndiyo iliyokuvuta ukaanguka.
Mimi ni mtumishi wa Mungu najua haya yote kwa sababu tunakutana na watu kama huyu wengi tu. Unaweza ukawa umeolewa na mwanaume mwema sana tu. Lakini akakutana na dada mwenye roho ya namna hii nakuambia kama mumeo hana nguvu za rohoni ni rahisi mno kujikuta anavutwa na huyo mwanamke na akaanguka naye kabisaa.
Na mumeo akakosa amani miaka yake yoote akijiuliza hivi ilitokeaje. Hata kwa wewe mwanaume ni vivyo hivyo. Unaweza oa mwanamke mzuri sana wa tabia, akikutana na jamaa kama huyo ninayekusimulia na mkeo wewe hutaki asali, hutaki amtumikie Mungu, Mungu ndani yake hayumo unafikiria kitatokea nini?
Nimeishawahi kukutana na wasichana tena wasomi tu wanaomba maombi yaani unamkuta binti anakusimulia tokea amefika chuoni tu hapo ana miaka mitatu kaishatembea kuanzia na wanafunzi wenziwe waalimu wafagiaji hapo chuoni, wajenzi hapo chuoni, wauza mgahawa, wauza duka siyo muuza duka nasema wauza duka, mpishi, nk.
Sitaniii nakuambia ukweli. Anakuambia yeye ndiye anawafuata akimfuata mwanaume tu lazima azini naye.
Ukiwasikikiza watu wa jinsi hiyo ndipo utalielewa Mungu asemavyo hivi. “Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba. Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda. Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu; Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu. Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake. Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.” (Mithali 7:18-27)
Zamani nilikuwa nawalaumu watu wazinzi na ninawahukumu mnoo. Unajua siku Mungu ananifundisha somo hili na kuanza kuona ninapolifundisha somo hili hasa kwa vijana wakike na wakiume nilipoanza kuona mapepo hayo yakilipuka kwa watu wengine na tukiyakemea na hao watu naona wengi wakianguka chini na kuzini na ardhi wengine wakitoa nguo ili wawe uchi ndipo nilipobadilika moyoni mwangu nikaanza kuwaonea huruma watu wenye tabia ya uzinzi hasa wadada.
Wadada wengi adui kawaonea mnoo, kama hujui ni rahisi kuwachukia mno na kuwatengenezea sheria na kila neno baya utawaita na hata kuwaandika nk. Lakini nakuambia ukweli ile roho au mapepo ya uzinzi ndiyo yanawabana na kuwakosesha mnoo.
Hapo nakufundisha elimu kubwa mno. Nikajifunza kwa nini Bwana Yesu alisema watenda dhambi ni watumwa wa dhambi. Sijui wewe hiyo nyumba ya Mungu yaani mwili wako nani anaumiliki? Fikiria mtu ana jeshi humo ndani yake ya mapepo ya uzinzi.
Tofauti yake na huyo Mgerasi ni kuwa huyu amevaa suti na anaendesha gari ni msomi hivi, ni kiongozi hivi, lakini ana mapepo mwilini labda chukulia matatu tu ya uzinzi?
Atajikuta akizini iwe kwenye hiyo gari ukimletea mabinti wa kazi anazini nao, ofisini anazini nao, umpeleke kanisani anazini na mtoto wa mchungaji, nk. Mpaka siku atakapopata ufahamu kuwa hii tabia si ya kawida.
Sasa naona umepata nuru hebu jingalie kama nilivyokuambia nitakuandikia mambo ya kufanya hebu angalia unafikiri huo mwili wako unavyokusumbua je! Ni mwili au ni roho? Kwa ujumla ukiwa na hii roho siyo rahisi kuitawala kama unavyoweza kuutawala mwili.
Ila usiogope uwe wazi tu. Ikiwa unaona hiyo ni roho usifiche niambie tu kuwa naona mimi nimebanwa hii ni roho ya uzinzi.
Naamini umenielewa kwa sehemu hebu tufuatane katika somo hili hapo mbeleni.
Leo nimekuandikia kwa urefu kidogo Mungu akusaidie usome na uelewe na uyafahamu haya.
Mungu akubariki
Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-
1. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org
2. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).
3. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”
4. Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”
5. DVDs 📀 au CDs 💿
6. VITABU.
NB: Wasiliana na Brigitha kwa namba +255 (0) 763 109 733, kupata VITABU, DVD & CD.
7. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.
8. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:- radio.mwakatwila.org
Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 (0) 754 849 924 Au +255 (0) 756 715 222
Wako
Mwl Steven & Beth Mwakatwila.
02/02/2019
No comments:
Post a Comment