Wednesday, April 29, 2020

Salamu – Juni, 2019

Salamu – Juni, 2019

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Tunamshukuru sana Mungu ambaye amekuwa pamoja nasi katika mwezi wa tano uliopita.

Tumekuwa na semina tatu kubwa ambazo tulifunga hema katika mikoa miwili. Tumekuwa na semina mkoa wa Songwe maeneo ya Vwawa na Tunduma. Pia tumekuwa na semina katika mkoa wa Rukwa pale Sumbawanga Mjini.

Zilikuwa ni semina nzuri mnoo.

Hebu tuendelee na salamu maalumu katika mwezi huu.

JIFUNZE KUTAKASA KILA TENDO LILILOANDIKWA KATIKA VITABU VYA MATENDO MBINGUNI NA DUNIANI

Hebu tuangalie eneo hili.

ONDOA KUMBUKUMBU HIZO ZILIZOKO KWENYE NAKALA HIZO ILI ZISIKULETEE MADHARA

Sikiliza, unaweza ukafanya dhambi fulani huko nyuma, mfano ulizini au uliua na ukaomba msamaha kabisa. Lakini lazima ujifunze kuifuta au kuiondoa hiyo dhambi kwenye kumbukumbu yoyote itakayokumbukwa hapa hapa duniani.

Kumbuka dhambi inapofanywa, kumbukumbu zake zinatunzwa hapa hapa duniani na huko mbinguni. Dhambi uliyoifanya inaweza kukufuata hapa duniani au wewe ukaifuata huko mbinguni kwa lugha nzuri utaikuta.

Ngoja nikupe mfano huu uone. Angalia mistari hii: “Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa BWANA. BWANA akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni. Ndipo mfalme akawaita Wagibeoni akawaambia; (basi Wagibeoni si wa wana wa Israeli, ila ni wa masalio ya Waamori; na wana wa Israeli walikuwa wamewaapia; lakini Sauli akatafuta kuwaua katika juhudi yake kwa ajili ya wana wa Israeli na Yuda;)” (2 Samweli 21:1-2)

Ukiisoma hiyo mistari utaelewa hiki ninachokufundisha. Angalia. Mfalme Sauli aliua hao watu, Sauli akafa na ikapita miaka mingi mnoo, siku moja njaa ikatokea katika taifa la Israeli. 

Njaa hiyo ikadumu miaka mitatu. Angalia kitu cha ajabu ambacho ndicho nataka nikutazamishe. Njaa hiyo chanzo chake ilikuwa ni dhambi ya damu ambayo Sauli aliimwaga.

Kumbuka Sauli hakuwepo aliishakufa. Cha kujifunza hapo ni nini? Ni hiki, dhambi hutunzwa katika nakala kama kivuli duniani na nakala kama halisi huko juu mbinguni. Hii dhambi iliandikwa mahali na ndiyo maana ikaifuata hiyo taifa la Israeli lililo chini ya utawala wa mfalme mwingine kabisa yaani mfalme Daudi tena rafiki wa Mungu.

Maana yake nini? Daudi hakushughulikia hizo nakala zilizotunza hizo kumbukumbu za dhambi iliyofanywa na aliyemtangulia.

Naamini kumbukumbu hizo zilitunzwa sehemu zote mbili. Sauli siamini kama alifanikiwa kuzifuta hizo kumbukumbu za damu ambazo alizimwaga katika zile nakala za kutunzia matendo maovu zilizoko mbinguni. 

Unaweza kuniuliza kwa nini unasema hivyo? Kwa mujibu wa Biblia agano la kale lilikuwa halina damu bora inayoweza kushughulikia hizo nakala za mbinguni.

Ukitulia tena unaona Sauli hakushughulikia nakala zinazotunza kumbukumbu za mambo duniani. Ndiyo maana dhambi iliyofanywa na mfalme ambaye alitumia nafasi ya ufalme wake kuua watu, dhambi hiyo ilikumbukwa katika ufalme wa Daudi na ikamfuata Daudi na ufalme wake yaani taifa zima la Israeli.

Dhambi ikitunzwa kwenye kumbukumbu za huku duniani fahamu zitawafuata watu walioko duniani na zitapitisha madhara makubwa sana.

Kumbukumbu za maovu yako zilizotunzwa mbinguni kama hazikushughulikiwa fahamu ndizo zitatumika kama ushahidi wa kukupeleka jehanum.

Kumbukumbu za dhambi zilizotunzwa kwenye nakala zilizopo duniani kama hazikushughulikiwa fahamu zitatumika kama ushahidi unaotafuta uhalali wa wewe kuadhibiwa ukiwa humu humu duniani.

Ngoja nikupe mfano mwingine labda utanielewa. Kuna mwaka ambao serikali ilifanya uamuzi wa kupitia vyeti vya wafanyakazi ambao wameajiriwa na serikali.

Unajua watu wengi sana walijikuta wamepoteza kazi na elimu zao kisa ni dhambi waliyoifanya zamani sana ilipokumbukwa katika nakala zilizotunza matendo ya uovu ambayo yaliwekwa dhahiri humu humu duniani.

Fikiria watu wengi walisahau kama waliifanya hiyo dhambi. Wengine waliokoka kabisa na kuwa watumishi wa Mungu. Bahati mbaya hawakujua namna ya kushughulikia kumbukumbu za dhambi yao hiyo walioifanya.

Fikiria cheti kilicholeta shida kilikuwa cha kidato cha nne. Mtu alisoma mpaka akachukua shahada mbili wengine wakawa madaktari n.k. Siku dhambi hiyo ilipowafuata tu wakajikuta wamekwama katika kila kona. Sikiliza jifunze katika kushughulikia mara kwa mara nakala zilizotunza hizo kumbukumbu zako.

Inawezekana kabisa ni dhambi ulizofanya wewe au walizofanya waliokutangulia. Yaani wazazi wako, viongozi waliokutangulia wewe ukachukua nafasi yao au ulizofanya wewe mwenyewe.

Unaweza kusema mbona kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake? Ni sawa, lakini lazima ujue kuwa kuna dhambi akiifanya mtu mwingine kumbukumbu zikikumbukwa, wanaoweza kupata madhara ni watu ambao yamkini hata wao hawakushiriki hiyo dhambi kabisaa.

Mfano: Mfalme Daudi hakuwaua hao watu, lakini Israeli yoote ilitumikia adhabu hiyo siku dhambi hiyo ilipokumbukwa. Hata watoto saba wa Sauli, waliitumikia dhambi ilipowafuata. Soma hicho kitabu chote cha 2 Samweli 21, utaona hiki ninachokuambia.

“Na kwa sababu hiyo hekima ya Mungu ilisema, Tazama, nitatuma kwao manabii na mitume, nao watawaua baadhi yao na kuwafukuza, ili kwa kizazi hiki itakwe damu ya manabii wote, iliyomwagika tangu kupigwa msingi wa ulimwengu; tangu damu ya Habili hata damu ya Zakaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na hekalu. Naam, nawaambieni ya kwamba itatakwa kwa kizazi hiki.
Ngoja nikupe mfano huu mwingie.” (Luka 11:49-51)

Fikiria kidogo kama damu za watu zikitakwa mikononi mwa hao ndugu maana yake kuna nakala zilizotunza kumbukumbu za maovu waliyoyafanya watu waliowatangulia hao watu.

Na dhambi hiyo iliwafuata hao watu ambao hawakuwepo kabisa Kaini alipokuwa amuua Habili na pia Zakaria alipouawa kati ya madhabahu na hekalu.

Naona sasa umenielewa ninapokuambia jifunze kushughulikia katika kuzitakasa hizo nakala zilizoko mbinguni na duniani zilizobeba kumbukumbu za uovu.

Mungu akubariki sana. Tuonane katika kona hii mwezi ujao.

Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo;
1.Website yetu ya www.makatwila.org

2. Youtube- Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU

3.Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga

4.Dvds au Cd

5.Vitabu
6.Kwa njia ya Redio mbalimbali Rungwe fm102.5 Kila siku Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku

na Baraka Fm107.5 kila siku ya jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku na Bomba fm 104.1 kila siku ya ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku
7: Unaweza kutupata kwenye redio yetu online ya. radio.mwakatwila.org
Kwa mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi. 0754849924-0756715222

Wako
Mr &Mrs Steven Mwakatwila

Tuesday, April 28, 2020

Salamu – Mei, 2019

Salamu – Mei, 2019 Nina wasalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo aliye hai. Tunamshukuru Mungu sana ambaye ametulinda na kutupatia mwezi huu wa tano. Ni neema kubwa. Nimekuletea tena salamu za mwezi wa tano. Kumbuka tuna salamu tunazotembea nazo zenye kichwa JIFUNZE KUISHI MAISHA YA UTAKASO Katika salamu za mwezi uliopita tulianza kujifunza eneo la JIFUNZE KUTAKASA KILA TENDO LILILOANDIKWA KATIKA VITABU VYA MATENDO MBINGUNI NA DUNIANI Na tuliangalia mistari hii. ” Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo. Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo.”(Waebrania 9:22-23) Ebu tusogee mbele kidogo. FAHAMU MATENDO YAKO UYATENDAYO YAPO YANAYOKUTANGULIA MBINGUNI NA WENGINE YANAWAFUATIA Angalia mistari hii. “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata.”(1Timotheo 5:24) Ukiisoma hiyo mistari utagundua kuwa dhambi inapofanywa na mtu, mtu huyo lazima ajue tendo hilo alilolifanya ovu litamtamgulia huko mbeleni. Atalikuta siku ile ya hukumu. Maana yake nini? Unaweza kupata maana nyingi tu, lakini moja ya maana ni hii ninayokuambia matendo ya mtu yanatunzwa huko mbinguni ambako ndiko sote tutaenda. Na matendo hayo unayoyafanya yanatunzwa kwa mtindo wa kuonekana yaani yanarekodiwa kama kwa video camera hivi. Biblia inasema siku ile ya mwisho matendo ya kila mtu yatakua dhahili. Angalia mistari hii. “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata. Vivyo hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.”(1Timotheo 5:24-25) Neno dhahili maana yake ni wazi wazi. Ni kuonekana, sasa unaposikia matendo yao dhambi zao zimewatangulia na zipo dhahili maana yake siku ya hukumu kila mtu matendo yake mabaya aliyoyafanya atayakuta kwenye hizo nakala zilizotunzwa huko mbinguni Sikiliza kuna maeneo mawili yanayotunza kumbukumbu za matendo ya watu. Moja ni mbinguni mbili ni duniani. Unajua huku duniani fahamu kuna kumbukumbu za matendo yako. Kunadhambi zilizokutangulia zingine zinakufuata maana yake ni hivi. Kuna nakara zinazotunza taarifa zako ziko mbinguni ukifa utaenda kuzikuta na kuna zitakazo kufuata maana yake ni nakara zilizotunzwa duniani. Unapofanya toba lazima ujue kushughulikia hizo nakala za pande zote mbili. Ngoja nikutafakarishe kidogo. Si unajua unaweza ukawa una copy mbili zinazofanana? Kunautofauti wa nakala halisi nanakala kivuli. Biblia inasema wazi kuwa kuna mambo ya mbinguni yaliyodhahili na ya duniani ambayo nikivuli au copy ya mambo yaliyoko duniani. Angalia mistari hii. “Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wo wote kuwakamilisha wakaribiao. Kama ndivyo, je! Dhabihu hazingekoma kutolewa; kwa maana waabuduo, wakiisha kusafishwa mara moja, wasingejiona tena kuwa na dhambi? Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.”(Waebrania 10:1-4). Ukiipitia hiyo mistari utagundua hiki ninachokufundisha. Damu ya mafahali au wanyama iliweza kushughulikia kufuta au kutakasa au kufunika matendo maovu yaliyofanywa na mtu huku duniani tu. Mbinguni walikua bado wakizitunza hizo kumbukumbu ingawa huku duniani zikiwa zimefutwa. Ninachotaka nikufundishe ni hiki. Jifunze kuomba maombi mara kwa mara kwa Mungu afute matendo yako mabaya yaliyoko kwenye nakala zote mbili. Yaani nakala za duniani ambazo zinaweza kukufuata, na nakala zilizoko mbinguni ambazo wewe zimekutangulia nawewe utazikuta huko mbinguni. Ebu tufuatane katika kona hii katika kipindi kijacho. Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo 1.Website yetu ya www.makatwila.org 2. Youtube- Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU 3.Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga 4.Dvds au Cd 5.Vitabu 6.Kwa njia ya Redio mbalimbali Rungwe fm102.5 Kila siku Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku na Baraka Fm107.5 kila siku ya jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku na Bomba fm 104.1 kila siku ya ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku 7: Unaweza kutupata kwenye redio yetu online ya. radio.mwakatwila.org Kwa mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi. 0754849924-0756715222 Wako Mr &Mrs Steven Mwakatwila

Salamu – Aprili, 2019

Salamu – Aprili, 2019 Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Naamini unaendelea vema. Nimekuletea mfululizo wa salama za mwezi. Kumbuka tunasalamu zenye kichwa .Ebu tusogee mbele kidogo j JIFUNZE KUISHI MAISHA YA UTAKASO JIFUNZE KUTAKASA KILA TENDO LILILOANDIKWA KATIKA VITABU VYA MATENDO MBINGUNI NA DUNIANI Sikiliza. Moja ya eneo ambalo unatakiwa ulijue na ulishughulikie ni hili la kufanya maombi mara kwa mara ya kuomba Mungu Roho Mtakatifu kwa kutumia Damu ya Bwana Yesu Kristo atakase matendo mafu au maovu ambayo yameandikwa au kutunzwa huko mbinguni. Biblia inatufundisha kuwa mbinguni kuna kazi ya kutunza kila matendo au maneno mabaya ambayo wanadamu wanayafanya na kuyasema. Angalia mistari hii. “Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo. Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo.”(Waebrania 9:22-23). Angalia kitu hiki, mbinguni kuna nakara ambazo zinatakiwa zisafishwe kwa damu. Katika agano la kalenakala hizo zilikua haziwezi kusafishika kwasababu ya upungufu wa ubora wa damu za wanyama ambazo zilitumika kufanyia utakaso. Kwa masna nzuri iko hivi. Huku duniani Mungu aliamuru matendo mafu yoote yatakaswe kwa damu. Kitu cha kujifunza hapo ni hiki. Damu za wanyama zilizotumika kufanyia utakaso zilishindwa kufanyia utakaso wa nakara zilizotunzwa mbinguni za matendo hayo hayo mabaya yaliyofanywa na watu. Maandiko yanasema hivi. “ambayo ndiyo mfano wa wakati huu uliopo sasa; wakati huo sadaka na dhabihu zinatolewa, zisizoweza kwa jinsi ya dhambi kumkamilisha mtu aabuduye, kwa kuwa ni sheria za jinsi ya mwili tu, vyakula na vinywaji na kutawadha kwingine kwingine, zilizoamriwa hata wakati wa matengenezo mapya. Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele. Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng’ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili; basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?”(Waebrania 9:9-14). Ukiipitia hiyo mistari utaona damu za hao wanyama hazikua na nguvu za kusafisha kila kitu. Hazikufanikiwa kusafisha nakala za matendo mafu ambazo zilikua zikitunzwa mbinguni. Angalia mfano Biblia inasema “Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo” Ebu tujiulize mbinguni kuna dhambi inayofanyika? Kama hakuna kwanini nakala zilizoko huko zisafishwe? Nini kilikua kikitunzwa humo kwenye hizo nakala? Sikiliza. Mbinguni wanatabia ya kutunzwa matendo yetu mbalimbali. Ndiyo maana unatakiwa ujifunze mno namna ya kujifanyia utakaso. Unaweza kujitakasa roho, nafsi, na mwili lakini usishughulikie nakala zilizo beba kumbukumbu ya matendo yako mafu ambazo zinatunzwa huko mbinguni. Naamini sasa umeanza kunielewa ninaposema jifunze kufanyia utakaso wa matendo yako mafu yaliyotunzwa mbinguni. Katika salamu za mwezi ujao tutaendelea kujifunza kiundani kidogo mahali hapohapo. Mungu akubariki tuonane katika sehemu hii mwezi ujao. Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo 1.Website yetu ya www.makatwila.org 2. Youtube- Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU 3.Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga 4.Dvds au Cd 5.Vitabu 6.Kwa njia ya Redio mbalimbali Rungwe fm102.5 Kila siku Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku na Baraka Fm107.5 kila siku ya jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku na Bomba fm 104.1 kila siku ya ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku 7: Unaweza kutupata kwenye redio yetu online ya. radio.mwakatwila.org Kwa mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi. 0754849924-0756715222 Wako Mr &Mrs Steven Mwakatwila

Saturday, April 11, 2020

SALAMU ZA PASAKA 2020

Na MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA

Ninawasalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo. Mimi na familia yangu tunamshukuru sana Mungu kwa wema wake kwetu hata kutupatia siku hii maalumu ambayo tunaadhimisha kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Hili ni tukio muhimu sana sana kwa wanadamu wote.

 SIKUKUU YA PASAKA YA MWAKA HUU NI TOFAUTI SANA NA SIKUKUU ZA PASAKA ZINGINE
Sikiliza, sikukuu ya pasaka ya mwaka huu imekuja katika mfumo ambao ulimwengu unapitia katika kipindi kigumu mnoo cha kukutana na maradhi ya Corona (COVID-19).

Watu wengi mnoo katika mataifa mbalimbali wameingia katika siku hii ya pasaka wakiwa wameamliwa kutokutoka nje ya nyumba zao. 
Hata wengi wanashindwa kwenda kwenye makusanyiko matakatifu ili kumfanyia Mungu ibada, wapo ndani hawajui nini kinaendelea huko nje.
Naona sasa umenielewa ninapokuambia sikukuu hii ni tofauti na sikukuu nyingine za pasaka.

Lengo langu mpaka kukuonyesha haya nina nia ya kutaka kukutia moyo. Maandiko yanatufundisha tuonapo mambo kama haya yakitukia tufanye nini.

JAMBO LA KWANZA: NI WAKATI WA KUCHANGAMKA
Angalia mistari hii: “Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika. Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.” (Luka 21:25-28)

Unapoipitia hiyo mistari utajifunza hiki ninachokuambia yaani changamka. Sikukuu ya Pasaka hii ndani yake imebeba fundisho hili kuwa Bwana Yesu Kristo yu karibu mlangoni. 

Kwa lugha nzuri zaidi ni wakati wa kuinuka na kutokujiruhusu ukate tamaa au uchoke. Ni wakati wa kujiweka sawasawa katika mfumo wa Imani yako. 

Mataifa yoote yanaishuhudia dhiki hii ya Corona, hofu imeikumba Dunia ghafla, watu wengi wamevunjika moyo, wengi hawana tumaini tena, uchumi wa mataifa umeanguka ghafla, uchumi wa mtu mmoja mmoja umeanguka ghafra.

Dunia imepoteza watu wengi mnoo tena muhimu mnoo kwa kipindi kifupi mnoo na hakuna ajuaye hii janga litaisha lini. Sikia maandiko yanasema mwonapo mambo kama hayo yakitokea ulimwenguni Basi changamkeni.

Changamkia maombi mpendwa, ondoa uvivu, changamkia Neno la Mungu, soma na sikiliza. Changamka katika utumishi uliopewa. Panga namna utakavyomtumikia Mungu katika kipindi hiki hiki.

Unajua ni rahisi ukafa moyo kisa mikutano ya injili imezuiliwa, semina zimezuiliwa, makusanyiko ya maombi yamezuiliwa, nk. Changamka mpendwa panga ratiba zako, tafuta mwongozo wa Roho Mtakatifu wa namna utavyowafikia watu katika kipindi hiki.

Si kipindi cha kulala kiutumishi. Unajua Mungu ana njia nyingi mnoo za kuwafikia watu? Bahati mbaya watu wengi hawakuwa na maandalizi kama siku wakikutana na hali kama hii inakuwaje?

Soma Biblia uone kama Bwana Yesu Kristo alikuwa na mfumo mmoja tu wa kuhubiri na kufundisha. Fikiria mchungaji unategemea kondoo waje katika jengo tu siku ya Jumapili na ghafla unakutana na hali kama hii?

Sijui wachungaji wangapi Watanzania wamejipanga namna ya kuchunga watu kwa mtindo wa namna hii? 
Kanisa halikuwa na maono ya namna hii, wainjilisti hatukuwa na maono ya namna hii, ndiyo maana utaona  baada ya mambo haya kutokea watumishi wengi wamevunjika mioyo. 

Hapana tunahitaji kuchangamka. Mwombe Mungu akupe maarifa ya namna ya kuwafikia watu na kuwachunga. Ni kipindi kingine Mungu anatupa shule kubwa hapo.

Soma uone wenzetu walitumikaje walipozuiliwa kwenda kwenye mikusanyiko, angalia nchi za wenzetu ambao mpaka leo hii walikatazwa katika nchi zao kuhubiri au kujenga majengo ya kuwakusanyia Wakristo na kuwachungia humo ndani.

Soma mchungaji uone ni mbinu gani wanatumia kuwachunga waaminio bila serikali zao kujua.
Kipindi hiki ndiyo cha kuchangamka sana. Ni kipindi cha kuhakikisha kanisa linabadili mfumo wa kuwaandaa waaminio bila kumtegemea mchungaji au mtumishi yeyote.

 Fikiria mchungaji hukuwaandaa waumini wako, kusoma Biblia, kuomba na kujisimamia, na inatokea mwezi mmoja tu hakuna kukutana na hao waumini unafikiri siku ya kukutana nao kuna Ukristo hapo?

Yes!!!! Naona moyoni mwangu kuchangamka kweli kweli katika kipindi hiki, kwa sababu naona kanisa kuanza kujenga imani kwa Bwana Yesu Kristo mfufuka kuliko kujenga imani kwa mtu, watu, dini, n.k.

 Kuna nchi nimesikia waaminio ambao zamani waliambiwa ni marufuku wao kuomba toba mpaka mtumishi awaombee, sasa imani imekuja ghafla kwa watumishi kuwaambia waaminio kuwa hata wao wanaweza kuomba toba huko huko nyumbani walikofungiwa.

Shida yangu ipo hapa je! Waumini hao waliandaliwa vema? Usifikiri ni rahisi mtu kuomba ikiwa hakuandaliwa kuomba, usifikiri ni rahisi mtu kumwamini Mungu kuwa amemsamehe kama hakuandaliwa mapema.

JAMBO LA PILI: INUA MACHO YAKO JUU AU IMARISHA IMANI YAKO KWA BWANA YESU KRISTO
Kama mpendwa ulikuwa hauko vizuri katika mfumo wa imani yako chukua hatua mpendwa ya kuimarisha imani yako vizuri kwa Bwana Yesu Kristo. Maandiko yanasema “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”

Sikiliza pasaka hii unatakiwa ujitathmini wewe mwenyewe moyoni mwako kiwango cha imani yako au unavyomtazama mwokozi wako unamtazama kwa kiwango kipi?
Fahamu Bwana Yesu Kristo anasema hivi: “walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?” (Luka 18:8B)

Bwana Yesu Kristo anapokuja je! Ataiona imani yako kwake? Umejenga imani yako wapi? Unajua ni rahisi kujenga imani yako kwa mapokeo, au dini, au watumishi, mume, mke, baba, huduma, n.k, na usiijenge hiyo imani yako kwa Bwana Yesu mfufuka.

Anza kujenga imani yako kwa Bwana Yesu Kristo si kwa kitu kingine mpendwa.

JAMBO LA TATU: BADILISHA MFUMO WA MAISHA YAKO; ONDOA TABIA MBAYA.
Ni kipindi ambacho kuanzia dakika hii uhakikishe unaishi maisha ya utakaso: “Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa. Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.” (Ufunuo 22:11-12)

Uyaonapo hayo, jifunze kuzidi kujitakasa. Kuna njia mbili kuu za kujitakasa, njia ya kwanza ni kwa Damu ya Bwana Yesu Kristo. Na njia ya pili wewe kutogusa vichafu, yaani dhambi.
Kiwango chako cha kuishi maisha safi kinatakiwa mpendwa ukiongezee yaani uzidi. Acha dhambi, ndiyo umeokoka na umeitwa hata umtumikie Bwana Yesu Kristo, lakini kumbuka Bwana yupo karibu mlangoni. 

Anataka akuone ukiwa mtakatifu, ondoa mwenendo wowote wa uovu. Ishi maisha ya kumpendeza. 

Nikutakie Sikukuu njema. Barikiwa.

Wako
Steven & Beth Mwakatwila

11/04/2020.

Thursday, April 9, 2020

8️⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU KATIKA ENEO LA MATATIZO YALETWAYO NA TAUNI

Na: MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA.

FUATANA NASI:- KWENYE APP,  FACEBOOK, INSTAGRAM, ONLINE RADIO 📻, WEBSITE, WHATSAPP & YOUTUBE Kwa links zilizoko hapa kwenye link hii:

KUPATA APP YETU “HUSONEMU (MWAKATWILA) APP”: (humo utapata masomo haya yote ninayokuletea darasani na mengine mengi) bonyeza link hapa.

🖊️  06 /04/ 2020.

Bwana Yesu Kristo asifiwe. Ninakukaribisha tena darasani ili tupate kujifunza somo hili muhimu. 

HIKI NI KIPINDI CHA NANE.

JAMBO LA NANE
H. JIFUNZE KUKIRI USHINDI KWA KINYWA CHAKO.

Mungu ili akuokoe katika majanga pia atataka kuangalia ukiri wako: “Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya. Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake naliona hasira, nikampiga; nalificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe. Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.” (Isaya 16-19)

Mungu anapokasirika na kuadhibu ili aponye fahamu ataangalia maneno yasemwayo. 
Angalia vizuri anasema atamponya huyo aliyepinga na kumletea amani kwa sababu Mungu anayaumba matunda ya midomo. 

ILI UTOLEWE KWENYE MAUTI LAZIMA UJIFUNZE KUKIRI HUO WOKOVU

Angalia hii mistari uone: “Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” (Mithali 18:20-21)

Katika kipindi hiki unatakiwa ubadilike katika kusema kwako. Anza kukiri huo wokovu usiseme  kwa kinywa chako kuwa utakufa.

Angalia mistari hii: “Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA.” (Zaburi 118:17)

Ukitaka upone majanga haya nakushauri jifunze kuukiri wokovu kutoka kwa Mungu. Angalia mistari hii: “Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!” (Warumi 10:10-15)

Naamini umenielewa mpendwa katika ujumbe huu ambao Roho Mtakatifu aliniwekea ndani ya moyo wangu na nikapata kibali cha kukushirikisha.
Mungu akubariki sana.

Tunapoachana nataka nikupe taarifa hii kuwa ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-

1. App yetu ya huduma yenye jina  “MWAKATWILA” utaipata Play Store kwenye link pale juu, ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

2. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

3. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

4. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya Facebook (f) "like" na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

5. Instagram ingia Instagram app halafu andika “steven-mwakatwila

6. DVDs 📀 au CDs 💿

7. VITABU.

NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

8. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

9. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 754 849 924 Au
+255 756 715 222

Wako
Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

🖊️ 06/04/2020.

7️⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE WOKOVU KATIKA ENEO LA MATATIZO YALETWAYO NA TAUNI

Na: MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA.

FUATANA NASI INSTAGRAM

FUATANA NASI:- KWENYE APP,  FACEBOOK, INSTAGRAM, ONLINE RADIO 📻, WEBSITE, WHATSAPP GROUPS & YOUTUBE; Kwa links zilizoko hapa kwenye link hii:

🖊️  04 /04/ 2020.

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana, Namshukuru Mungu mimi na familia yangu ni wazima. Nimekuletea somo darasani, karibu tujifunze.

HIKI NI KIPINDI CHA SABA

 JAMBO LA SABA
G. JIFUNZE KUTOKUISHI KWA HOFU ISIYOFAA

Sikiliza ili leo hii upate kuokolewa na Mungu katika majanga ambayo chanzo chake ni tauni iliyoachiliwa na Mungu, ikiwa wewe ni kuhani na umewajibika kwa sehemu yako unatakiwa uhakikishe unaondoa hofu moyoni mwako ya kukutana na mauti hiyo iliyobebwa na tauni iliyoachiliwa na Mungu

                          KUNA HOFU AU WOGA WA AINA MBILI

Unaposoma maandiko matakatifu utaona ndani ya Biblia tunafundishwa kuwa kuna hofu za aina mbili; 

➖HOFU INAYOTOKA KWA MUNGU
Angalia mistari hii: “Basi tukiijua hofu ya Bwana, twawavuta wanadamu; lakini tumedhihirishwa mbele za Mungu. Nami natumaini ya kuwa tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia.” (2 Wakorintho 5:11)

Angalia na mistari hii: “Tazama, nitatia roho ya hofu ndani yake, naye atasikia kivumi, na kuirudia nchi yake mwenyewe; nami nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.” (2 Wafalme 19-7)

Hofu ni roho. Ukiipitia hiyo mistari hiyo utaona kuwa kuna hofu ya Bwana, ambayo hutoka kwa Mungu kabisa. Hofu hii Mungu huitumia kwa kazi nyingi tu. 

Moja ya kazi ya hofu hii ni kuwafanya wanadamu wamwogope Mungu na kuacha matendo yao mabaya. 

Angalia mfano huu angalia na mistari hii: “Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli. Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu. Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha. Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii. Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao. (Zaburi 78:31-35)

Ukiipitia hiyo mistari utagundua kuwa Mungu anapoona wanadamu wamezidisha uovu juu ya nchi huchukua hatua ya kuwatiisha hao watu kwa jambo fulani ambalo ndani yake huibeba roho hiyo ya hofu na hofu hiyo maandiko husema huwashitua watu na watu hao ndipo huona umuhimu wa kumtafuta Mungu na kuacha njia zao mbaya.

                    TAUNI HUBEBA HOFU YA MUNGU NDANI YAKE

Mungu ana akili nyingi mnoo ya kutuvuta kwake ukiona majanga kama ya ya tauni fahamu ndani yake majanga haya hubeba hofu ya Mungu ndani yake. 
Watu wanapokufa kwa tauni unajua ndipo wanadamu wengi huanza kumkumbuka Mungu na kumwogopa? 

Wanadamu wengi huingia katika mashaka makubwa na mifadhaiko mingi mioyo yao hubeba huzuni n.k. Biblia inasema huzuni hubeba hofu na pia zipo huzuni za aina mbili pia

Angalia mistari hii: “Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu.Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.” (2 Wakorintho 2: 7-11)

Ukiipitia hiyo mistari utaona kuwa huzuni pia hubeba hofu. Hofu itokayo kwa Mungu huibeba  huzuni pia itokayo kwa Mungu. Mungu anapotuhuzunisha wanadamu kwa kutuletea hofu fahamu anachokitafuta ni kuona hao wanadamu wanatubia matendo yao.
Biblia inasema haya majanga yanapotokea huleta faida, angalia anasema: “Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto;”
Mtu yeyote yule mwenye akili timamu hawezi kuendelea kufanya jambo ambalo anajua kabisa mwenzie kaadhibiwa tena kwa kuuawa. Mwenye akili ataliacha hilo jambo haraka sana. Na ataogopa kuendelea kulifanya. 

Leo hii hofu hii ya Corona imewavuta watu wengi waanze kumkumbuka Muumba wao. Hata wale wanaomkumbuka wanajipanga vizuri kweli kweli. Ehehee!!

Ngoja nikukumbushe kitu. Kumbuka zamani ulipokuwa shule ya msingi siku ya mkaguo na iwe zamu ya yule mwalimu ambaye anafahamika kwa ukali mpaka shule ya tatu ambayo hajawahi hata kufundisha?

Wanafunzi woote siku hiyo huingiwa na hofu na kila mmoja utaona muda wa dakika chache tu alivyojifanyia usafi; iwe kwa mate, kwa kula kucha, kama nywele hakuchana na kichanio hakipo unajua hutafuta chelewa zinapangwa na kuwa kichanio siku hiyo mpaka nywele zionekane sawa.

Mungu anapowajilia wanadamu kwa mtindo huo wa kuwatia adhabu fahamu ndani yake hutaka kuona watu wakiwa na hofu ya kumwogopa.

Biblia inasema hivi: “Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.” (Zaburi 4:4)

Hii ni hofu ya Mungu inayotufanya sisi tusifanye dhambi. Ukimhofu Mungu au kumcha fahamu huwezi kutenda dhambi. Na hofu hii inaweza kubebwa na taarifa uliyoipata kuwa Mungu amewafanyia jambi fulani watu waliotenda dhambi, huwezi wewe ukatenda dhambi wakati wenzio wamepigwa.

Biblia inatufundisha kuwa tunatakiwa tuwakemee watu wadumuo kutenda dhambi mbele za watu ili watu wengine waogope. Angalia mistari hii: “Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.” (1 Timotheo 5:20)

Kama Mungu anampa mwanadamu maarifa haya unafikiri yeye hawezi kuwaogopesha watu kwa kuyafanya mambo kama yayo hayo? Mungu huleta tauni ili tu kutujengea sisi wanadamu hofu ya kutokudumu katika kutenda maovu. 

➖HOFU ILETAYO MAUTI AU MABAYA
Pia Biblia inatufundisha kuwa kuna hofu ambayo chanzo chake si Mungu. Na hofu hiyo inaweza kumsababishia huyo mwenye hofu kukipata kitu hicho kibaya anachokiogopa.
Angalia mistari hii: “Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.” (Mithali 10:24) 
Ukiipitia hiyo mistari utagundua kuwa. 
Haikupasi ndugu kuwa na hofu ya kupatwa na tauni. Kwa mujibu wa mistari hiyo tunafundishwa kuwa ili tusipatwe na tauni au jambo baya tunatakiwa tuhakikishe hatukiogopi hicho kitu.

Sikiliza mwogope Mungu, usiogope kitu kingine. Angalia hii mifano: “Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu. Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.” (Mithali 3:24-25)

Unapoona kuna mambo kama hayo wewe mpendwa unatakiwa usiingize hofu yoyote. 
JENGA IMANI YA KUOKOLEWA KATIKA JANGA HILI

Kumbuka unapopata hofu ni rahisi kujikuta unakutana na hicho, unachokiogopa.
Mfano, angalia umesikia habari za Corona, moyoni mwako unalitazamaje hili jambo? Wewe ni kuhani, mwombezi unatakiwa uhakikishe unajenga imani moyoni mwako ya kuokolewa na Mungu katika janga hili.

Usiogope na kujaa mashaka na kukosa amani kisa eti umesikia Corona inaua wazee, wagonjwa, n.k.

Ili uokolewe unatakiwa ujifunze kutokuwa na mashaka. (SINA MAANA USICHUKUE HATUA YA KUNAWA, NK) Ninachotaka kukujengea ni hiki usiogope amini kuokolewa hata kama ukikutana nao.

Kwa nini uwaze kufa wakati kuna watu wameugua Corona na wamepona? Kwa nini ufikiri utaambukizwa wakati kuna watu wengi tu wapo katika nchi iliyojaa Corona na hawajaambukizwa?

                  KAA MBALI NA MTU AKULETEAYE MANENO YA HOFU

Biblia inasema hivi: “Tena maakida na waseme zaidi na watu, wawaambie, Ni mtu gani aliye hapa tena mwenye hofu na moyo mnyonge? Aende akarudi nyumbani kwake, isije mioyo ya nduguze ikayeyuka mfano wa moyo wake.” (Kumbukumbu la Torati 20:8)

Ukiipitia hiyo mistari utaona hiki ninachokuambia. Mtu ambaye ana moyo wa hofu haifai kukaa naye karibu. Atakuambukiza hiyo roho ya kuogopa.

                        HOFU AU MASHAKA NI SUMU YA IMANI

Unapomwomba Mungu akuokoe na tauni unatakiwa ujenge imani ya kuokolewa wewe na nyumba yako na taifa lako. Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo. 
Jenga uhakika moyoni mwako ya kuwa Mungu ameokoa. SIYO ATAKUOKOA NASEMA AMEKUOKOA. Ukijenga imani hiyo fahamu hautazama ndani ya tauni. 

Angalia mifano hii: “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano. Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake. Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho. Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu. Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope. Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.  Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?” (Mathayo 14:22-31)

Ukiipitia hiyo mistari utakigundua hiki ninachokuambia. Kilichomfanya Petro azame ni hofu ya maji. Fikiria alianza kutembea juu ya maji. Fikiria mwokozi yupo na ndiye amemwambia njoo yeye aliona shaka. 

Shaka ndiyo sumu ya imani. Na sisi tunaokokewa kwa imani. Hata hili janga tunaokolewa kwa imani.

Ondoa woga amini umeokolewa mpendwa!!! Usiangalie unasikia nini wangapi wamekufa wangapi wameambukizwa n.k.

Naona watoto wa Mungu wameacha hata kufanya kazi ya kuwaingizia kipato kisa eti Corona. Usihofu ondoa masikio yako kusikia habari za kukutisha. Binafsi nilimwelewa haraka Rais wetu aliposema kuhusu kutokuhofu au kutiishwa tuchape kazi.

Fanya kazi zako kama kawaida, panga mipango yako kama kawaida. Mwenye kwenda shamba nenda shamba. Ngoja nikuchekeshe, unaweza leo hii ukapita kwenye vumbi hivi au ukapita kwenye eneo watu wanapaka ukuta rangi, ni rahisi kujikuta una mafua sasa hapo Eheheee!!!!! Unashangaa mpendwa anaanza kuwasumbua watu tu na wauguzi. 

“Ohoo! Nahisi ninao!!!” Sikiliza ondoa hofu mpendwa yamkini ni mafua ya kawaida tu. Fikiria ndiyo umekutana na mtu ana mafua tu. Hapo sasa Ehehee!!

Usishangae mtu ndiyo anashuka kwenye gari au bajaji kisa anaogopa Corona, ukifikia hali hiyo mpendwa wewe sasa ni utumwa na ni mtu asiye na imani kwa Mungu wake.

Hebu tumalizie leo kwa mistari hii ili usiogope:  “Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita. Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi. Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;  Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?” (Zaburi 56:1-4)

Angalia na mistari  hii: “Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini. Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo. Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao. Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana, Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri, Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe. Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki. Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.” (Zaburi 91:1-11)

Sikiliza keti na Mungu kaa chini ya uvuli wake yaani jiachie kwake utaokolewa na tauni mpendwa. Usihofu sasa. Fanya unayoweza kufanya lakini jenga matumaini yako kwake. 

Bwana Yesu Kristo kukuokoa. 

Mungu akubariki sana. 

Nikukumbushe kidogo kuwa ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-

1. App yetu ya huduma yenye jina  “HUSONEMU (MWAKATWILA)” utaipata Play Store kwenye link pale juu, ambapo kuna masomo mengi sana hapo.

2. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

3. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

4. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya Facebook (f) "like" na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”

5. Instagram ingia Instagram app halafu andika “steven-mwakatwila

6. DVDs 📀 au CDs 💿

7. VITABU.

NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.

8. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

9. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 754 849 924 Au
+255 756 715 222

Wako
Mwl Mr & Mrs Steven Mwakatwila.

🖊️ 04 /04/ 2020.