2⃣4⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE KUISHINDA DHAMBI YA UZINZI
Na: MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA
FUATANA NASI:- KWENYE APP, FACEBOOK, INSTAGRAM, ONLINE RADIO 📻, WHATSAPP, WEBSITE & YOUTUBE, Kwa links zilizoko kwenye HII LINK hapa:
KUPATA APP YETU “HUSONEMU (MWAKATWILA) APP” BONYEZA LINK HII HAPA:
🗓 28 Machi, 2019
Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Naamini unaendelea vizuri. Nimekuletea mfululizo wa somo nililokuahidi kukufundisha. Kumbuka katika kipindi kilichopita nilikuonyesha eneo lile la namna ya kufanya ikiwa utaona dalili za kuwa kuna pepo la uzinzi ndani ya mwili wako.
Nilikufundisha kuwa jambo la kufanya ni kulitoa tu hulo pepo.
Ngoja tuendelee mbele kidogo pepo hatakiwi atulizwe, anatakiwa atolewe ndani ya mtu. Na pia asipewe nafasi ya kumrudia huyo mtu tena.
Bwana Yesu Kristo siku moja alikutana na mtu mwenye pepo angalia alipokuwa analitoa alilipa amri ya kutokumrudia huyo mtu tena. “Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena. Akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka; naye akawa kama amekufa; hata wengi wakasema, Amekufa. Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama.” (Marko 9:25-27).
Ukiipitia hiyo mistari utaona wazi kuwa Bwana Yesu Kristo alitoa amri ya huyo pepo asimrudie huyo mtu tena. Unapoisoma hiyo mistari unaona umuhimu wa sisi leo tunapoyatoa hayo mapepo yaliyo ndani ya watu tujifunze kutoa amri kwa hayo mapepo kutowarudia hao watu tena.
Kumbuka huduma hii inabebwa na mamlaka ya ufalme wa Mungu. Kwa hiyo kinachoamrishwa kitatii kile kilichosemwa na mtoa amri kwa sababu amebeba mamlaka.
Mara nyingi tunajisahau sana tunapoyatoa hayo mapepo ndani ya watu kuyawekea amri hii ya kutokuwarudia hao watu tena. Unajua ulimwengu wa roho unaheshimu mno kile kilichosemwa kimamlaka. Pepo hatoki kwa kupenda anaamriwa na pia lazima aamriwe asirudi hapo alipotolewa.
Unaposoma maandiko unaona sababu nyingi tu zinazopelekea mtu kurudiwa na pepo.
Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Naamini unaendelea vizuri. Nimekuletea mfululizo wa somo nililokuahidi kukufundisha. Kumbuka katika kipindi kilichopita nilikuonyesha eneo lile la namna ya kufanya ikiwa utaona dalili za kuwa kuna pepo la uzinzi ndani ya mwili wako.
Nilikufundisha kuwa jambo la kufanya ni kulitoa tu hulo pepo.
Ngoja tuendelee mbele kidogo pepo hatakiwi atulizwe, anatakiwa atolewe ndani ya mtu. Na pia asipewe nafasi ya kumrudia huyo mtu tena.
Bwana Yesu Kristo siku moja alikutana na mtu mwenye pepo angalia alipokuwa analitoa alilipa amri ya kutokumrudia huyo mtu tena. “Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena. Akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka; naye akawa kama amekufa; hata wengi wakasema, Amekufa. Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama.” (Marko 9:25-27).
Ukiipitia hiyo mistari utaona wazi kuwa Bwana Yesu Kristo alitoa amri ya huyo pepo asimrudie huyo mtu tena. Unapoisoma hiyo mistari unaona umuhimu wa sisi leo tunapoyatoa hayo mapepo yaliyo ndani ya watu tujifunze kutoa amri kwa hayo mapepo kutowarudia hao watu tena.
Kumbuka huduma hii inabebwa na mamlaka ya ufalme wa Mungu. Kwa hiyo kinachoamrishwa kitatii kile kilichosemwa na mtoa amri kwa sababu amebeba mamlaka.
Mara nyingi tunajisahau sana tunapoyatoa hayo mapepo ndani ya watu kuyawekea amri hii ya kutokuwarudia hao watu tena. Unajua ulimwengu wa roho unaheshimu mno kile kilichosemwa kimamlaka. Pepo hatoki kwa kupenda anaamriwa na pia lazima aamriwe asirudi hapo alipotolewa.
Unaposoma maandiko unaona sababu nyingi tu zinazopelekea mtu kurudiwa na pepo.
Sababu nyingine ambayo inaweza kumfanya pepo wa uzinzi arudi kwa mtu aliyetolewa pepo ni HOFU KWA HUYO MTU ALIYETOLEWA PEPO.
Watu wengi waliotolewa pepo huwa wamebeba hofu ya kuona watarudiwa na hali hiyo tena. Maandiko yanasema kile unachokihofu ni rahisi sana kukupata. “Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.” (Mithali 10:24).
Unapotolewa pepo hilo jenga ndani yako imani isiyo na hofu kuwa litakurudia hata ukiona dalili za kuwaka tamaa ya uzinzi. Kumbuka mwili unaweza kuwasha tamaa ya kufanya tendo la ndoa.
Sasa wengi wanapokutana na hali hii ya mwili kuwaka tamaa badala ya kuushughulikia mwili huanza kufikiria ile hali yao ya kwanza ya pepo la uzinzi imewarudia.
Hubeba hofu na hofu hiyo huwaharibu katika imani na mwisho kweli huyo pepo huwarudia. Ukifanyiwa huduma ya namna hii jenga imani usiwe na mashaka kuwa halijatoka, au litarudi hata uonapo dalili yoyote.
Shetani ni mjaribu na mwongo, atakujaribu tu na kukudanganya kwa kukutisha kwa kukuonyesha kuwa hajatoka. Akiona imani uliyonayo kuwa huna pepo hilo tena atakuacha.
Unajua mtu mwenye hofu au mashaka maana yake hajaamini. Nenda kaombewe ukiambiwa na waombaji hao kuwa pepo ametoka amini. Ukiambiwa bado hajatoka usisite kuendelea kuombewa mpaka upate uhakika kuwa ametoka.
Ukiambiwa ametoka jenga imani hapo usihofu kuwa hajatoka hata kama alisumbua sana kutoka.
Sababu nyingine ni DHAMBI.
Watu wengi waliotolewa pepo huwa wamebeba hofu ya kuona watarudiwa na hali hiyo tena. Maandiko yanasema kile unachokihofu ni rahisi sana kukupata. “Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.” (Mithali 10:24).
Unapotolewa pepo hilo jenga ndani yako imani isiyo na hofu kuwa litakurudia hata ukiona dalili za kuwaka tamaa ya uzinzi. Kumbuka mwili unaweza kuwasha tamaa ya kufanya tendo la ndoa.
Sasa wengi wanapokutana na hali hii ya mwili kuwaka tamaa badala ya kuushughulikia mwili huanza kufikiria ile hali yao ya kwanza ya pepo la uzinzi imewarudia.
Hubeba hofu na hofu hiyo huwaharibu katika imani na mwisho kweli huyo pepo huwarudia. Ukifanyiwa huduma ya namna hii jenga imani usiwe na mashaka kuwa halijatoka, au litarudi hata uonapo dalili yoyote.
Shetani ni mjaribu na mwongo, atakujaribu tu na kukudanganya kwa kukutisha kwa kukuonyesha kuwa hajatoka. Akiona imani uliyonayo kuwa huna pepo hilo tena atakuacha.
Unajua mtu mwenye hofu au mashaka maana yake hajaamini. Nenda kaombewe ukiambiwa na waombaji hao kuwa pepo ametoka amini. Ukiambiwa bado hajatoka usisite kuendelea kuombewa mpaka upate uhakika kuwa ametoka.
Ukiambiwa ametoka jenga imani hapo usihofu kuwa hajatoka hata kama alisumbua sana kutoka.
Sababu nyingine ni DHAMBI.
Nataka nikutazamishe hapo dhambi kwa aina mbili, kuna dhambi ikiyotangulia kufanywa na dhambi aifanyayo mtu huyo baada ya kutolewa pepo.
Nianze kwa dhambi iliyotangulia kufanywa. Kuna watu ambao wamejikuta wakiwa na mapepo kwa sababu ya kuyafungulia mlango wao wenyewe kwa viapo au maangano fulani.
Wanaweza wakawa ni wao wenyewe au waliowatangulia, watu wa namna hiyo hujikuta wamefungiwa au kubanwa na hayo mapepo kihalali.
Biblia inasema hivi “Je! Aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?” (Isaya 49:24).
Umeona hapo? Kuna wafungwa waliofungwa kihalali kabisaa, kwenye ulimwengu wa roho kuna watu wamefungwa na vifungo mbalimbali kihalali. Maana yake kuna makosa yalifanyika au maagano fulani yalifanyika na hayo ndiyo yanayotumika kumpa shetani na mapepo uhalali wa kuwabana au kuwafungia watu hata tabia mbaya zilizobebwa na mapepo.
Sasa unaweza kuombewa pepo akatoka lakini akarudi haraka kwa sababu bado ana uhalali wa kumtesa huyo mtu kwa sababu ya kutokutubiwa au kuondolewa kitu kile kinachompa uhalali huyo pepo wa kumfuatilia huyo mtu.
Ngoja nikupe mfano huu. Kuna ndugu alikuwa amewekewa ndani ya tumbo lake hirizi. Aliwekewa na mganga kwa kutumia maji aliyoyaoga tu. Mganga huyo akamwambia nimekuwekea zindiko tumboni.
Sasa siku mimi nakutana naye anaumwa ili nimwombee pepo akalipuka. Ilinichukua zaidi ya masaa nane kumwombea ili hilo pepo limwachie mpaka alipokunya hiyo hirizi.
Alipoitoa hiyo hili kwa kupitia njia ya haja kubwa tu akafunguka. Uhalali wa hilo pepo kumbana na kumfuatilia huyo mtu ulikuwa katika ile hirizi aliyokuwa nanyo ndani ya tumbo lake.
Unajua siku ile nilijifunza kitu kikubwa sana. Kuna watu walipewa vitu na wachawi au waganga wa kienyeji vinaonekana vya kawaida tu kumbe ndani yake vimebeba mapepo mengi tu. Sasa unaweza kukemea hilo pepo litoke, pepo litatoka lakini kama kile alichopewa huyo mtu hakijashughulikiwa fahamu pepo anapata uhalali wa kurudi hapo kwa sababu kibebeo chake kikichombeba huyo pepo na kumwingia huyo mtu bado kipo
Cha msingi hapo wewe mwenye hiyo shida yaani hilo pepo usisite kumweleza ukweli huyo mtumishi chanzo cha wewe kuingiliwa na hiyo roho. Watu wengi hujitahidi sana kuficha mambo yao mabaya. Hilo linawagharimu sana.
Unakuta mtu anakueleza leo kimoja ndani ya vitu kumi ambavyo ilitakiwa akueleze. Watumishi wengi wakikuona siyo mkweli au haupo wazi kwao wanakuacha. Wakifikiri wewe hupendi kufunguliwa.
Eleza ukweli, mwingine anasema kwani Mungu hawezi kumuambia huyo mtumishi? Si kila mtumishi ni nabii. Nabii anaona anasikia kwa uwazi mno mambo ya ulimwengu wa roho. Na si kila kitu nabii pia huonyeshwa. Huyo nabii pia ni mtu anaweza ona na kusikia asielewe kabisaa.
Sasa fikiria wewe unayejua ukweli hauusemi unaficha. Unapokuwa mkweli fahamu ndipo unapowekwa huru mapema mnoo. Unapomueleza mtumishi dhambi yako au yenu iliyofungulia mlango wa pepo kuwafuatilia ni rahisi kufanya toba iliyonyooka.
Mnapofanya toba na kuachilia damu ya Yesu Kristo mahali palipokosewa ili iondoe hiyo dhambi ndipo uhalali wa hayo mapepo kukumiliki unapokosa nguvu na yanapotolewa ni ngumu kuludi kwasababu hayana haki tena ya kukumiliki.
Ndiyo maana mkianza kufanya maombi ya toba tu utaona mapepo yanaanza kupata shida mno mahali hapo. Nimeona mara nyingi tu. Mnapokuwa katika kusanyiko lenye watu wengi, mnapoanza kufanya maombi ya namna hiyo tu, usishangae kuona mapepo yanaanza kuangaika.
Mengine yatapiga kelele mengine kuanguka chini yatafanya kila aina ya fujo. Toba ya kweli inamwondolea shetani uhalali wa kuwamiliki watu. Dhambi ndiyo chanzo kikubwa cha kumpa adui uhalali wa kummiliki mtu na kumtesa.
Naamini umenielewa. Angalia je! Kuna uhalali wowote umpao shetani kukumiliki? Tubia hapo. Mweleze huyo mtu anayekuombea nini unaona kinampa adui nafasi ya kukumiliki. Ndiyo itakuwa rahisi pepo kutoka au kutokukurudia.
Mungu akubariki sana
Wako
Mwl Steven & Beth Mwakatwila
Nianze kwa dhambi iliyotangulia kufanywa. Kuna watu ambao wamejikuta wakiwa na mapepo kwa sababu ya kuyafungulia mlango wao wenyewe kwa viapo au maangano fulani.
Wanaweza wakawa ni wao wenyewe au waliowatangulia, watu wa namna hiyo hujikuta wamefungiwa au kubanwa na hayo mapepo kihalali.
Biblia inasema hivi “Je! Aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?” (Isaya 49:24).
Umeona hapo? Kuna wafungwa waliofungwa kihalali kabisaa, kwenye ulimwengu wa roho kuna watu wamefungwa na vifungo mbalimbali kihalali. Maana yake kuna makosa yalifanyika au maagano fulani yalifanyika na hayo ndiyo yanayotumika kumpa shetani na mapepo uhalali wa kuwabana au kuwafungia watu hata tabia mbaya zilizobebwa na mapepo.
Sasa unaweza kuombewa pepo akatoka lakini akarudi haraka kwa sababu bado ana uhalali wa kumtesa huyo mtu kwa sababu ya kutokutubiwa au kuondolewa kitu kile kinachompa uhalali huyo pepo wa kumfuatilia huyo mtu.
Ngoja nikupe mfano huu. Kuna ndugu alikuwa amewekewa ndani ya tumbo lake hirizi. Aliwekewa na mganga kwa kutumia maji aliyoyaoga tu. Mganga huyo akamwambia nimekuwekea zindiko tumboni.
Sasa siku mimi nakutana naye anaumwa ili nimwombee pepo akalipuka. Ilinichukua zaidi ya masaa nane kumwombea ili hilo pepo limwachie mpaka alipokunya hiyo hirizi.
Alipoitoa hiyo hili kwa kupitia njia ya haja kubwa tu akafunguka. Uhalali wa hilo pepo kumbana na kumfuatilia huyo mtu ulikuwa katika ile hirizi aliyokuwa nanyo ndani ya tumbo lake.
Unajua siku ile nilijifunza kitu kikubwa sana. Kuna watu walipewa vitu na wachawi au waganga wa kienyeji vinaonekana vya kawaida tu kumbe ndani yake vimebeba mapepo mengi tu. Sasa unaweza kukemea hilo pepo litoke, pepo litatoka lakini kama kile alichopewa huyo mtu hakijashughulikiwa fahamu pepo anapata uhalali wa kurudi hapo kwa sababu kibebeo chake kikichombeba huyo pepo na kumwingia huyo mtu bado kipo
Cha msingi hapo wewe mwenye hiyo shida yaani hilo pepo usisite kumweleza ukweli huyo mtumishi chanzo cha wewe kuingiliwa na hiyo roho. Watu wengi hujitahidi sana kuficha mambo yao mabaya. Hilo linawagharimu sana.
Unakuta mtu anakueleza leo kimoja ndani ya vitu kumi ambavyo ilitakiwa akueleze. Watumishi wengi wakikuona siyo mkweli au haupo wazi kwao wanakuacha. Wakifikiri wewe hupendi kufunguliwa.
Eleza ukweli, mwingine anasema kwani Mungu hawezi kumuambia huyo mtumishi? Si kila mtumishi ni nabii. Nabii anaona anasikia kwa uwazi mno mambo ya ulimwengu wa roho. Na si kila kitu nabii pia huonyeshwa. Huyo nabii pia ni mtu anaweza ona na kusikia asielewe kabisaa.
Sasa fikiria wewe unayejua ukweli hauusemi unaficha. Unapokuwa mkweli fahamu ndipo unapowekwa huru mapema mnoo. Unapomueleza mtumishi dhambi yako au yenu iliyofungulia mlango wa pepo kuwafuatilia ni rahisi kufanya toba iliyonyooka.
Mnapofanya toba na kuachilia damu ya Yesu Kristo mahali palipokosewa ili iondoe hiyo dhambi ndipo uhalali wa hayo mapepo kukumiliki unapokosa nguvu na yanapotolewa ni ngumu kuludi kwasababu hayana haki tena ya kukumiliki.
Ndiyo maana mkianza kufanya maombi ya toba tu utaona mapepo yanaanza kupata shida mno mahali hapo. Nimeona mara nyingi tu. Mnapokuwa katika kusanyiko lenye watu wengi, mnapoanza kufanya maombi ya namna hiyo tu, usishangae kuona mapepo yanaanza kuangaika.
Mengine yatapiga kelele mengine kuanguka chini yatafanya kila aina ya fujo. Toba ya kweli inamwondolea shetani uhalali wa kuwamiliki watu. Dhambi ndiyo chanzo kikubwa cha kumpa adui uhalali wa kummiliki mtu na kumtesa.
Naamini umenielewa. Angalia je! Kuna uhalali wowote umpao shetani kukumiliki? Tubia hapo. Mweleze huyo mtu anayekuombea nini unaona kinampa adui nafasi ya kukumiliki. Ndiyo itakuwa rahisi pepo kutoka au kutokukurudia.
Mungu akubariki sana
Wako
Mwl Steven & Beth Mwakatwila
- 28-03-2019