Wednesday, March 13, 2019

2⃣2⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE KUISHINDA DHAMBI YA UZINZI

2⃣2⃣ MAMBO MUHIMU UNAYOTAKIWA UYAFANYE ILI UPATE KUISHINDA DHAMBI YA UZINZI

Na: MWL STEVEN & BETH MWAKATWILA

KUPATA APP YETU “HUSONEMU (MWAKATWILA) APP” BONYEZA LINK HII HAPA:

FUATANA NASI:- KWENYE APP, FACEBOOK, INSTAGRAM, ONLINE RADIO 📻, WHATSAPP, WEBSITE & YOUTUBE, Kwa links zilizoko kwenye HII LINK hapa:

🗓 13 Machi, 2019

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. Naamini unaendelea vizuri mimi na familia yangu hatujambo tunamshukuru Mungu atutunzaye na kutupigania.

Nakuletea mwendelezo wa hili somo nililokuahidi kukufundisha ili upate ufahamu wa namna unavyoweza kuishinda dhambi ya uzinzi.

Katika somo lililopita nilikuonyesha  mlango au chanzo cha saba ambacho kinaweza kuwa mlango wa pepo kumwingia mtu.

Hebu tusogee mbele nikuonyeshe chanzo kingine kinachoweza kufungulia mlango wa mtu kuingiliwa na pepo hasa la uzinzi nacho ni

CHANZO CHA NANE NI; TABIA MBAYA YA KUFANYA UZINZI AU UASHERATI

Sikiliza ikiwa wewe ni mtu mwenye tabia ya uzinzi fahamu ni rahisi sana kuvamiwa na pepo la uzinzi.

Fahamu linaitwa pepo la uzinzi, sasa kama mwili wako huo wewe mwenyewe umeshindwa kuudhibiti katika eneo la kuzipinga tamaa zake na moja ya tamaa ya mwili ni uzinzi, fahamu kwa kupitia hiyo tabia ya uzinzi iliyobebwa mwilini mwako  pepo la uzinzi linaweza itumia hiyo tabia kukuingia ili kukufanya uwe mzinzi kweli kweli.

Unajua unapofanya uzinzi au unapojamiiana na mtu awe wa kike au kiume  usifikiri ni mwili wako tu unaolifanya hilo tendo, fahamu hata roho inashiriki. Maandiko yanasema hivi “Watu wangu hutaka shauri kwa gongo lao, na fimbo yao huwahubiri mambo; maana roho ya uzinzi imewakosesha, nao wamekwenda kuzini mbali na Mungu wao.” (Hosea 4:12).

Angalia maandiko yanasema roho ya uzinzi imewakosesha. Hiyo roho si mwili, kwa mujibu wa hiyo mistari tunapata ufahamu kuwa kuna ushirika kabisa wa roho ya mtu au mapepo katika suala zima la mtu kufanya ngono.

Ukilijua hili ni rahisi sana kuelewa pia mistari hii isemayo “Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;” (1 Wakorintho 6:15-19)

Ukisoma hiyo mistari utagundua kuna mahusiano makubwa kati ya mwili na roho katika eneo hili la tendo la ndoa. Mwili huu unamilikiwa na roho yako na Roho Mtakatifu angalia sasa ikiwa wewe unafanya zinaa fahamu ni rahisi zaidi roho au pepo la uzinzi likaumiliki mwili wako kwa sababu unapofanya hilo tendo hata roho yako ina sehemu ya ushiriki wa tendo hilo.

Roho Mtakatifu anapoumiliki mwili wa mtu fahamu hatapenda kuona mtu huyo anafanya uzinzi, kwa sababu Roho Mtakatifu ametupa utaratibu wa kuoa na kila mtu alieoa kwa kufuata utaratibu anapolifanya hilo tendo mwili wake hauwi najisi kwa sababu kalifanya kihalali.

Mtu anapolifanya hilo tendo nje ya utaratibu fahamu anaungana na mwili wake na huyo anayefanya naye hicho kitendo, sasa hebu fikiri huyo unayeungana naye anapepo la ngono au uzinzi?

Sikiliza watu wengine hujikuta wakiungana na roho mbaya au pepo la uzinzi kwa kupitia kujamiana au kuzini tu. Si mnakuwa hapo mnaachana na Roho Mtakatifu aumilikie mwili wako?

Unakuwa unakaribisha mmiliki mwingine wa mwili naye ni shetani. Shetani hawezi kujigawa na kuwa ndani ya kila mtu anachofanya ni kuyatuma mapepo ili yawaingie watu hao waliofanya maamuzi ya kuzini na kumwondolea Roho Mtakatifu uhalali wa kuimiliki miili yao wanakuwa wanaungana na hao wazinio na ni rahisi sana hapo kujikuta unaungana au kupokea roho au pepo la uzinzi.

Sikiliza watu wengi wanaofanya tendo la ndoa kinyume cha maumbile au wale wanaosagana au kufanya punyeto unajua wanakuwa katika hatari kubwa sana tena mnooo kuvamiwa na pepo hili la uzinzi.

Watu wengi walio na mapepo mbalimbali unapowauliza mfumo wa maisha yao hasa eneo hili la uzinzi utashangaa wengi waliingiliwa walipoanza kuzini na kuzini kwa mitindo hiyo ya kunyume cha maumbile au kusagana au  ushoga au kufanya punyeto.
Sikikiza nikuambia ibada za kishetani au ibada za kipagani unajua ndani ya hizo ibada wanaruhusu watu kuyafanya hayo.

Unajua ni kwanini wanafanya zinaa? Sikiliza wanafanya hivyo ili kuyafungulia mlango mapepo  au mashetani kuwaingia.

Kama unafikiri nakutania wewe fuatilia mahali popote ambapo kunafanyika mambo mabaya angalia mazingira hayo utagundua ni mazingira yanayojengwa ili kuchochea mno uzinzi.

Wewe nenda kwenye mikusanyiko yoote ya ibada za kishetani utaona huko watu wanakaa uchi au nusu uchi ili tu kuwatengenezea hao walioko hapo tamaa ya uzinzi tu.

Angalia wanavyocheza, angalia wanavyosema angalia wanavyotazamana, angalia wanavyokaa utaona ni kuchochea uzinzi tu angalia nyimbo zao wanazoimba ni mapenzi tuu na kuchochea uzinzi tuuu.

Unajua ni kwa nini uzinzi ndiyo unachukua nafasi ya kwanza hapo? Ni kwa sababu ndiyo mlango unaoyaruhusu mapepo kuwaingia hao watu na kuwatawala na kuwatengenezea tabia mbaya.

Mungu anapotuambia kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, ikimbieni zinaa anajua kabisa kuwa ukiendekeza zinaa tu mwili wako hauwi tena hekalu la Roho Mtakatifu unakua hekalu la mapepo.

Shetani akitaka kukuharibia masomo, biashara, kazi, heshima yako utumishi wako unajua atakachokifanya ni kukusukuma mnoo uingie kwenye tabia ya uzinzi tu, akikupata hapo amekupiga pakubwa mnoo.

Ndiyo njia anayoweza kukuingizia mapepo yatakayokuvurugia mnooo. Hata kama hajakuingia lakini yatakujeruhi tuuuu nakuambia.

Yatajeruhi ndoa kama si kuiua, yatajeruhi akili kama si kuziua nk. Biblia inasema hivi “Je! Mtu aweza kuua moto kifuani pake, Na nguo zake zisiteketezwe?Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto, Na nyayo zake zisiungue? Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake; Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia. Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake. Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika.” (Mithali 6:28:33)

Ukiipitia hiyo mistari utaona namna shetani anavyowajeruhi watu kwa kupitia uzinzi tu. Mapepo yanapomtafuta mtu ili yamjeruhi au kumtesa au kumharibia yanaweza mtegea kwenye kona hiyo ya uzinzi tu.

Ngoja nikuambie kitu unaweza usikaliwe na hilo pepo la uzinzi baada ya kuzini, lakini litaacha jeraha fulani tu. Lazima likutandike tu, dhambi ni dhambi iwe uongo nk. Lakini hazifanani kwenye eneo la madhara yake.

Uzinzi unamadhara makubwa mnoo nakuambia. Watu wengi wamejeruhiwa we acha tu. Siku moja Roho Mtakatifu   alinifundisha ni kwa nini au nini chanzo cha ndoa nyingi leo kuingia kwenye migogoro. Unajua chanzo kikubwa ni jeraha hili la uzinzi?

Wanandoa wengi mno chanzo kikubwa  cha ugomvi wao kimefungwa hapo tu. Utasikia ohooo mume wangu au mke wangu si mwaminifu. Maana yake anakuambia jeraha la ndoa yako ni zinaa aliyoifanya mke wangu au mume wangu.

Sikiliza wengi hapo huachana wengine hutengana. Pepo la uzinzi ni haribifu kweli kweli wa ndoa za watu. Ukigundua kuwa kuna jeraha yaani huwezi samehe una uchungu mnoo anza kuliona hilo pepo kwanza kabla ya kumwangalia mumeo au mkeo.
Usipokaa vizuri tu usishangae litakuvamia na wewe utaanza ghafla kufikiri kutoka kwenye ndoa yako ili ukazini nje ya ndoa. Unafikiri mawazo hayo chanzo chake ni nini? Ni hilo pepo tu linakutengenezea wewe tabia hiyo hiyo ya uzinzi.

Ndiyo hapo kesho unasikia mke wa fulani mzinzi, unamwuliza anasema ALIANZA YEYE KUTOKA NJE YA NDOA NA MIMI NIKAFUATA!!!! Au utaona pepo anakushauri achana na mumeo dai talaka au achana na mkeo dai talaka ili ukaolewe au kuoa mwingine. Aisee ee kumbe unasakiziwa hapo tabia ya uzinzi tu.

Usipolitazama pepo utamtazama mkeo au mumeo na mtaachana au kutengana tu. Ikimbie zinaa ili pepo la uzinzi au roho ya uzinzi usiipe nafasi ya kukuingia au kukujeruhi.
Angalia watu wengi leo hii wametoa mimba kisa uzinzi angalia alivyojeruhiwa, wengine hawana watoto na usishangae hawatapata kabisaa kisa pepo hili tu limewatengenezea jeraha baya kweli, liliwaingiza kwenye zinaa likawashauri watoe likawapigia hapohapo.
Fuatilia maisha ya watu walioua kwa kutoa mimba. Utashangaa ni watoro usoni pa ardhi, wanaishi maisha ya ajabu ajabu kama watu wasio na kikao duniani. Hawana amani kabisaa, waliotubu wamejikuta wamekaa na fadhaiko maisha yao yoote.

Unajua ukijeruhiwa ukipona jeraha unabaki na kovu kulingana na kiwango cha jeraha kilivyokuwa. Fikiria ulizini halafu ukapata mimba ukaitoa na unaishi bila mtoto au kuolewa au kuoa?

Ni sawa umetubu dhambi hiyo lakini kovu litakuwepo tu yaani kumbukumbu zitakuja tu, utafikiria aisee nisingezini yasingenikuta haya, aisee nisingetoa ileee mimba huenda ningekuwa na mtoto anayenifariji leo.

Hali hiyo ndiyo inayoitwa fedheha isiyofutika. Naona unanielewa sasa ninapokuambia kuhusu mlango huu wa zinaa unavyoweza kupitisha roho mbaya au mapepo ya uharibifu katika maisha ya mtu.

Siku moja nilikuwa nawaza namna ya watu wengi niliokuwa nao wakike na wakiume yaani niligundua wengi wamekufa hawapo. Na walikufa na umri mdogo sana. Kisa uzinzi tu.
Nilianza kuangalia fulani nini kilimuua niligundua ni UKIMWI tu, chanzo ni mlango huu huu tu. pepo la mauti lilipitia mlango huu kuwa walipolifungulia mlango wa kwa kuzini tu. Kila mtu atakufa, lakini wengine wanakufa kwa sababu mwili umechakaa tu.

Biblia inasema UMEISHA NGUVU ZAKE!!!! Na nguvu hizo huisha kutokana na UMRI WAPENDWA? Maandiko yanasema sabini kwa themanini.

Sasa angalia hao ninaowazungumza ni wengi mnoo, unaweza kusema unajuaje walikufa kwa UKIMWI? Sikiliza UKIMWI haunaga siri upo wazi hata watu waseme ni kisukari watu watajua si figo ni UKIMWI. Ninavyosema hivi usifikiri nafurahia.

Najisikia huzuni sana moyoni mwangu. Naona namna ya watu wengi tunakosa siri hizi na adui anawaangamiza kirahisi sana kwa kupitia tendo la zinaa la dakika kumi tu.
Ikimbie zinaa mpendwa yaani usijiamini wala kuiendekeza tabia hii utapata jeraha au mapepo yatakuingia tu. Biblia inasema usiwaendee wenye pepo na kuzini nao. “Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.Jitakaseni basi, iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.” (Mambo ya Walawi 20:6-7).

Ukiipitia hiyo mistari utapata tafsiri nyingi tu, moja ya tafsiri ni kitendo cha kuyauliza mapepo au kuongozwa na mapepo mbele za Mungu ni sawa na uzinzi. Lakini tafsiri nyingine ni hii ninayokuambia kuwa unapozini unaungana na yule mtu.

Sasa sikia, unapozini na mtu mwenye pepo ni rahisi ukajikuta unajiunganisha na hayo mapepo aliyonayo. Fahamu si kila mtu aliyewahi kuzini basi kapokea mapepo hapana nasema ni rahisi kuyapokea.

Ila unapozini fahamu hayo mapepo yasipokuingia lazima tu yatakuwa yamekujeruhi mahali fulani. Kama siyo ugonjwa basi ni jeraha la ndoa kuvunjika, akili kupigwa au kutoaminika.

Wewe fanya uzinzi leo hii huku ukiwa umeokoka utashangaa utatubu, lakini jeraha lako fahamu hautaaminika. Ukihubiri watasema leo yule mwanamke amehubiri sana usishangae mmoja atauliza yupi? Watasema yule mzinzi.

Ukisikia hivyo jipe moyo tu ni sehemu ya kovu, wewe sogea mbele. Lakini kwa nini ujitengenezee haya yooote? IKIMBIE ZINAA nakuambia.

Unajua hata ndani ya ndoa. Ukizini ukatubu fahamu umejitengenezea jeraha au kovu la kutokuaminika nakuambia. Mungu atakuamini ila watu au huyo mumeo au mkeo usishangae hakuamini tena.

Ukichelewa tu atafikiri ulipitia koloni lako hilo. Ngoja nikupe mfano huu. Kuna wanandoa walipokuwa wanaingia kuoana walizini, na hawataki kutubu au kutengeneza, unajua kwa kutokutubu kwao tu, ndipo mapepo yanapopata mlango wa kuwabamizia hapo hapo.

Nakushauri usizini na huyo mchumba wako, pepo litawaletea madanganyo kuwa si mtaoana? Sawa mtaoana lakini fahamu tendo hilo lisipotengenezwa tu, adui atawapigia kwa kutumia mlango huo huo.

Anaweza huko mbele yenu akaivunja hiyo ndoa msishangae hamuelewani, mnagomba wee hamaminiani, sikiliza mwenzio atakuaminije wakati mnaficha siri ya uzinzi mlioufanya? Shetani atautumia mlango huo kuwanong’oneza moja moja kuwa huyu mzinzi anaficha kama mlivyoficha uzinzi mlioufanya nyuma si mwaminifu huyu.

Hapo hapo maelewano kwenu yanaanza kuvunjika. Akichelewa sokoni nafsi iliyojeruhika inakuambia si uliwahi zini naye? Kwanza ulimkuta bikira? Eheheee!! Akirudi tu mkeo ugomvi, wivu nk mwisho ndoa kuvunjika.

Ikimbie zinaa. Vunja mahusiano mabaya na mwanaume au mwanamke yeyote yule. Kama unataka kumuoa muoe kihalali, usikubali mwanaume anayekushawishi uzini naye, mwanaume wa namna hiyo ni hatari kwako hebu jipange vizuri. Msichana anayejileta kwako na unaona wazi anataka uzini naye nakushauri mkimbie ni hatari kwako.

Kama uliwahi zini na huyo mumeo au mkeo kabla hamjaoana mkiwa kwenye uchumba nawashauri mkaufunge mlango huo mapema kwa toba, ungameni hiyo dhambi yenu.
Naamini umenielewa.

Ukihitaji masomo yetu unaweza kuyapata kwa njia hizi zifuatazo:-

1. Tovuti yetu ya www.mwakatwila.org

2. YouTube - Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).

3. Facebook ingia katika hiyo tovuti au website yetu utaona alama ya facebook(f) like na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika  “SOMA NENO LA MUNGU”

4. Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”

5. DVDs 📀 au CDs 💿

6. VITABU.
NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, kupata VITABU, DVD & CD.

7. Kwa njia ya REDIO:- Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
➖Rungwe FM 102.5 Kila siku ya Jumapili  saa tatu mpaka saa nne usiku.
➖Baraka FM 107.7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
➖Bomba FM 104.1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.

8. Unaweza kutupata kwenye ONLINE RADIO yetu:-  radio.mwakatwila.org

Kwa Mawasiliano zaidi Utatupata kwa namba hizi:-
+255 754 849 924 Au +255 756 715 222

Wako
Mwl Steven & Beth Mwakatwila.
13/03/2019

No comments:

Post a Comment